Hatua za kumuanzishia mtoto wa miezi sita chakula cha ziada

  • Hatua hizo zimegawanyika katika wiki tatu.
  • Mtoto huanza kupewa vijiko viwili hadi kufikia robo kikombe akifikisha mwaka mmoja.

Arusha. Lishe ni miongoni mwa mahitaji muhimu katika ukuaji wa mtoto ikimuwezesha kukua vyema na kumuepusha na magonjwa.

Katika miezi sita ya mwanzo wataalamu wa lishe hushauri mtoto apewe maziwa ya mama pekee bila kuchanganya na chochote ili kumpatia virutubisho vinavyohitajika katika hatua hiyo ya ukuaji.

Mwongozo wa lishe kwa watoto wadogo uliotolewa na Taasisi ya Chakula na Lishe (TFNC) unabainisha kuwa baada ya miezi sita ya mwanzo mtoto mchanga anahitaji chakula cha ziada ili kumpatia virutubisho ambavyo hupungua katika maziwa ya mama kadri mtoto anayokuwa.

“Vyakula vya nyongeza vinahitajika ili kumpatia mtoto nishati, vitamini na madini ambayo maziwa ya mama hayatoshelezi kadri mtoto anavyoendelea kukua,” umesema muongozo wa TFNC.

Mwongozo huo umebainisha kuwa mtoto anatakiwa kupata angalau makundi matatu ya chakula kwa kila mlo kati ya kundi la wanga, vyakula vya jamii ya kunde, mafuta na sukari, matunda na vile vyenye asili ya wanyama.

Hata hivyo, vyakula hivyo vya ziada hupaswa kuongezwa kwa hatua kadhaa ili mtoto aweze kuzoea na kurahisisha umengenywaji wake katika mfumo wa chakula wa mtoto.

Daktari Reinfrida Ngairo kutoka Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) ambaye pia ni mkufunzi wa lishe ya mama na mtoto ameimbia Nukta Habari kuwa hatua hizo zimegawanyika katika wiki tatu.

Ni muhimu kuzingatia uzito sahihi wa chakula cha mtoto ili aweze kuoata nishati na virutubisho vingine vya muhimu.Picha/Haakaa.

Wiki ya kwanza

Daktari Ngairo anasema mtoto anayeanzishiwa vyakula vya ziada huanza kupewa vyakula vyepesi (vya maji maji) kwa kiwango kidogo kisichozidi vijiko vitatu kwa siku mbili hadi tatu za mwanzoni.

“Lengo katika wiki ya kwanza ya kuanzisha chakula ni ku ‘introduce’ (kuitambulisha) tu ladha… kwa hiyo akila hata vijiko vitatu tu vinatosha akitaka zaidi ni sawa mpe zaidi na mlo mmoja unatosha kwa wiki ya kwanza.” ameongeza Dk Ngairo.

Vyakula hivyo ni pamoja na matunda yaliyopondwa na kuchanganywa na maziwa ya mama, maziwa ya kopo, au supu  kama ndizi, parachichi, papai, embe na tikiti huku siku ya tatu na kuendelea mzazi akiruhusiwa kumpa mtoto uji mwepesi wa nafaka moja ikiwemo mahindi, mtama, ulezi au uwele

“Kuchanganya nafaka zote kwa pamoja, unauchosha mfumo wa tumbo na mtoto anaweza hata asiweze pata virutubisho vyote vnavyohitajika…

kuanzia siku ya tatu ile anapoanza uji unaweza anza pia vyakula vingine mfano bogalishe, mtori, rojo la karoti, viazi, mboga majani na viazi lishe,” amesema Dk Ngairo.

Wiki ya pili

Katika wiki ya pili baada ya mtoto kuzoea chakula Dk Ngairo anashauri kumuanzishia vyakula vinavyoweza kuleta mzio mara moja kwa siku ikiwemo karanga, samaki, kiini cha yai, ufuta na aina nyingine.

“Kwa hiyo hapa unaweza mpa mtoto asubuhi mtori wa supu ya samaki umeweka mnofu kdogo wa samaki ukasaga…unafaya hivi siku mbili au tatu mfululizo ili ujue kama kitampa shida au la,” ameongeza Dk Ngairo.

Wataalamu wa afya wanashauri mtoto apate angalau aina tatu za makundi ya chakula.Picha/Felix Hospital.

Wiki ya tatu

Kuanzia wiki ya tatu hadi mtoto atakapofikisha mwaka mmoja unaruhusiwa kuchanganya vyakula mfano ndizi, kiazi, supu na mboga za majani pia kumpa uji wa nafaka mbili, mbegu na karanga.. 

Mtoto anakiwa kupewa vyakula hivyo mara tatu au nne kwa siku pamoja na asusa kama sharubati nzito na matunda kati ya mlo na mlo bila kusahau kunyoshwa kila anapohitaji.

Mwongozo wa TFNC unabainisha kuwa kadri mtoto anavyoendelea kukua anatakiwa kumaliza kikombe au kibakuli cha ujazo wa mililita 250 kwa mlo mmoja huku akiendelea kuacha vyakula laini sana kwenda vyakula vilivyopondwa hadi kufikia vyakula vyenye vipande vya kutafuna

Dk Ngairo amewataka wazazi kuzingatia kutoweka chumvi wala sukari katika chakula cha mtoto hadi anapofikisha umri wa mwaka mmoja ili kulinda figo ya mtoto na kusaidia mtoto asipoteze hamu ya kula.

Hakikisha vyombo vya mtoto vinaoshwa ipasavyo huku chakula kikipikwa katika hali ya usafi ili kumuepusha na magonjwa pamoja na kuzingatia mbinu bora za ulishaji.

New coffee standard opens markets for Tanzanian farmers

  • Regenerative Agriculture Certification launched this week by Rainforest Alliance.
  • The certification is aimed at restoring soil health, protecting biodiversity, and improving the livelihoods of smallholder farmers.

Dar es Salaam. Tanzanian coffee farmers could gain higher incomes and more resilient harvests after the launch of a new Regenerative Agriculture Certification, a global program aimed at restoring ecosystems in tropical regions while strengthening farmer livelihoods.

The certification announced on September 9, 2025 by Rainforest Alliance, an international non-profit organization, works to restore the balance between people and nature  for both to thrive in harmony.

According to the organization, the certification is aimed at restoring soil health, protecting biodiversity, and improving the livelihoods of smallholder farmers who produce the bulk of the world’s coffee.

The initiative comes at a time when climate change, pests, and environmental degradation are cutting yields and threatening rural incomes.

In Tanzania, where coffee is a key export and source of income for thousands of households in Kilimanjaro, Mbeya, and Ruvuma, the certification is expected to provide both market access and higher earnings for farmers who adopt regenerative practices.

The Rainforest Alliance says the new standard will give farmers and companies a clear, science-based way to measure their progress. Certified farms will be evaluated across five areas: soil health and fertility, climate resilience, biodiversity, water stewardship, and farmer livelihoods. 

Products that meet the requirements will bear a new regenerative seal, expected to appear on coffee packages starting in 2026.

Senior Director for East and Southern Africa at the Rainforest Alliance, Julius Ng’ang’a says the certification represents a shift in how markets support agriculture.

“Markets need to move beyond a ‘do no harm’ mindset to one that repairs and restores,” Ng’ang’a says. “Now is the time to transition to a new model of agriculture, one where every cup of coffee gives back more than it takes from the land and the people who care for it.”

Coffee is a key export and source of income for thousands of small farmers, higher yields and market access is key in improving livelihoods. Photo | Daily News.

Recent study on regenerative coffee investment case by TechnoServe shows regenerative farming practices can improve income by up to 20% to 30%. 

For Tanzanian producers, this could mean more stable earnings even as weather extremes and global market shifts affect coffee supply. 

Independent auditors will assess farms, and only those meeting the standard will be allowed to use the seal.

The certification also responds to growing consumer demand for sustainable products. For companies, sourcing regenerative coffee strengthens supply chains and supports environmental, social, and governance (ESG) goals. For buyers, the seal offers assurance that their purchase is helping both farmers and ecosystems.

The Rainforest Alliance has begun implementing the program in Brazil, Costa Rica, Mexico, and Nicaragua. Certified coffee from these countries is expected to reach shelves in 2026, with Tanzania and other African producers encouraged to join early to secure market advantages.

Zifahamu aina za zabibu na matumizi yake

  • Ni pamoja na zabibu zisizo na mbegu zinazofaa kukaushwa kuwa kavu.

Zabibu ni tunda lenye mvuto wa kipekee linalotumiwa duniani kote kwa njia mbalimbali. Iwe ni kuliwa kama tunda bichi, kutengeneza mvinyo au kukaushwa. Kila mtu na matumizi yake.

Tunda hili dogo liko katika mnyororo wa thamani wa tamaduni za chakula, afya na biashara, likiwa chanzo kizuri cha lishe, nishati na hata kipato kwa wakulima.

Hata hivyo, zabibu hazifanani kwa umbo na muonekano. Kwa nini? Kwa sababu ya utofauti wa mazingira na matumizi yake. 

Kwa mujibu wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), zabibu zimegawanyika katika makundi makuu matatu: za kutengenezea mvinyo,  za kuliwa kama matunda na zabibu za kukaushwa (raisins)

Utamu wa zabibu siku zote hutofautiana kulingana na aina ya zabibu. Picha/ Canva

Katika makala hii, utazifahamu aina hizi kwa undani zaidi kuanzia sifa zake hadi matumizi yake halisi. 

1. Zabibu za kutengenezea mvinyo

Zabibu hizi huchangamkiwa zaidi kwenye sekta ya uzalishaji wa vinywaji vya pombe, hasa mvinyo mwekundu na mweupe. 

Hutumiwa katika viwanda vya mvinyo duniani na hupandwa kwenye maeneo yenye hali ya hewa isiyo na joto kali wala baridi kali na mvua ya wastani

Nchini Tanzania, aina maarufu ni Makutupora nyekundu, Syrah, na Chenin nyeupe. Aina nyingine zinazotumika ni pamoja na ‘Cabernet Sauvignon’, ‘Merlot’, ‘Chardonnay’, Tempranillo na Airén.

Zabibu hizi huwa na tunda lenye juisi nyingi na ganda jembamba. Pia huwa na kiasi kikubwa cha sukari, ambayo ni muhimu kwa utengenezaji wa pombe kwa njia ya kuchachua.

Kwa kawaida, zabibu hizi haziliwi moja kwa moja kwa sababu ladha yake ni kali au chachu hivyo hupitia usindikaji ili kutoa mvinyo wenye ubora wa kimataifa, kulingana na aina ya zabibu na eneo la uzalishaji.

Zabibu za Cabernet Sauvignon asili yake ni Bordeaux ambako imekuwepo tangu karne ya 18. Picha/Canva.

2. Zabibu za kuliwa kama matunda

Hizi ni zabibu zinazopendwa kwa ulaji wa moja kwa moja bila kupitia usindikaji wowote. 

Huuzwa kama tunda sokoni na mara nyingi hupatikana katika maduka au masoko ya matunda.

Aina maarufu nchini ni Makutupora nyeupe, ‘Regina’, ‘Black Rose’, ‘Rosso’ ‘Crosso’, na ‘Alphonce Lavallee’. 

Zabibu ya Concord mara nyingi huitwa ‘Zabibu ya Marekani’ kwa sababu aina hii ilitengenezwa ili kuwapatia Wamarekani zabibu iliyofaa kwa hali zao za kilimo za kienyeji. Picha/ The Tree Center.

Aina za kimataifa ni pamoja na ‘Concord’, ‘Niagara’, ‘Everest Seedless’, ‘Edelweiss’, na ‘Bluebel’.

Zabibu hizi huwa na nyama nyingi, juisi kidogo na ganda gumu kiasi, zina kiwango cha chini cha sukari ukilinganisha na zabibu za mvinyo.

Zabibu za Niagara zilianza kuuzwa kibiashara mwaka wa 1882 na tangu wakati huo zimekuwa maarufu sana. Picha/FR.

Kwa sababu ya muonekano wake wa kuvutia, ladha tamu, na muundo wake thabiti, aina hizi hupendwa na walaji wa rika zote, hususan watoto.

Wakati wa kula huchanganywa na matunda mengine katika saladi au kwa matumizi ya moja kwa moja majumbani.

3. Zabibu za kukaushwa (raisins)

Hizi ni zabibu zinazolimwa mahsusi kwa ajili ya kukaushwa na kutumika baadaye kama kitafunwa au kiungo katika vyakula. Hutumika kwenye maandazi, keki, mikate, pilau na hata chakula cha watoto. 

Baadhi ya aina zinazopatikana ni ‘Beauty Seedless’, ‘Ruby Seedless’, ‘Halili Belly’, ‘Kismis Creven’, na ‘Cotton Candy’

Ukila hii zabibu kijani yenye maji, utaelewa kwa nini ni maarufu sana licha ya kuwa na ladha kama ya pipi ya pamba (cotton candy) l ni nzuri kwa kiafya. Picha/FR.

Za kimataifa ni pamoja na ‘Black Raisins’, ‘Currants’, ‘Sultanas’, ‘Flame Raisins’ na ‘Golden Raisins’.

Majina haya ya zabibu yametokana na asili ya sehemu zinapopatikana.

Zina umbo dogo, ganda jembamba na hazina mbegu, hali inayorahisisha ukaushaji wake kuwa wa haraka. Baada ya kukaushwa, huwa na ladha tamu zaidi na hudumu kwa muda mrefu. 

Zabibu kavu (raisins) zina kiwango cha chini cha mafuta ya asili na zina virutubisho vyenye afya. Picha/ Canva.

Raisins hupendwa kwa matumizi ya kila siku na ni chanzo kizuri cha nguvu kwa watoto, wanafunzi, na watu wanaofanya kazi nyingi za kushughulisha mwili.

Wewe unachagua aina ipi ya zabibu?

Njia za kumsaidia mtoto wako kupenda hisabati

  • Ni pamoja na kumpongeza na kumnunulia vitabu na programu za kielimu.
  • Mueleze mtoto umuhimu wa hisabati katika maisha yake ya kila siku.

Dar es Salaam. Somo la hisabati limekuwa kama ugonjwa usio natiba kwa wanafunzi wa ngazi mbalimbali za elimu nchini Tanzania. 

Hili limekuwa likijidhirisha katika matokeo ya mitihani ya kitaifa. Ufaulu wa wanafunzi katika somo hili umekuwa wa chini zaidi kuliko masomo mengine. 

Mathalani, katika matokeo ya kidato cha nne mwaka 2024 yaliyotolewa na Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA), ni asilimia 25.35 ya watahiniwa waliofanya mtihani wa hisabati, ndio walifaulu kwa kupata daraja A hadi D. 

Hiyo ni sawa kusema karibu robo tatu (wanafunzi 7 kati ya 10) walifeli somo hilo. Pia umefaulu huo wa mwaka jana umeshuka kutoka asilimia 25.42 iliyorekodiwa mwaka 2023. 

Suala hili la kufanya vibaya kwa wanafunzi katika somo la hisabati, limekuwa likiibua maswali mengi yasiyo na majibu miongoni mwa wazazi, walimu na wadau wa elimu. Baadhi ya wadau wanapendekeza uitishwe mjadala wa kitaifa kutafuta suluhu ya kudumu kuwawezesha wanafunzi kufanya vizuri katika soko hili. 

Mchambuzi wa masuala ya elimu na mwandishi wa vitabu, Richard Mabala amewahi kuiambia Nukta Habari (nukta.co.tz) kuwa suluhu ya pamoja itakayohusisha makundi yote kwenye jamii, inaweza kutoa mwelekeo mpya wa hisabati na kuwafanya wanafunzi wengi walipende somo hilo. 

Wadau wengine wa elimu wanasema mbinu shirikishi za ufundishaji zinaweza kusaidia wanafunzi kupenda somo hilo. 

Picha hii imetengenezwa kwa Akili Unde ikiwa lengo ni kukuonyesha namna unavyoweza kushirikiana na mwanao kuhakikisha anaelewa soma la hesabu.

Mwalimu wa hisabati kutoka Shule ya Sekondari Aga Khan Mzizima jijini Dar es Salaam, Veronica Sarungi, anasisitiza kuwa inawezekana kumfanya mwanafunzi kupenda hisabati kwa kutumia mbinu sahihi ikiwemo kutokumkatisha tamaa mtoto pale anapokuwa amefanya vibaya katika somo hilo. 

Ni kawaida kwa wazazi, walimu na hata wanafunzi wenzao kuwatisha watoto kwa kauli kama “Hisabati ni ngumu” au “Wewe huwezi hesabu.” 

Mwalimu Veronica anasema kauli hizo zina athari mbaya kwa watoto, kwani huwafanya kujiwekea vikwazo vya kisaikolojia na kuamini kuwa hawana uwezo wa kufanikisha somo hili. 

Badala ya kuwatia hofu, ni muhimu kuwahamasisha watoto kwa kuwatia moyo hata wanapokosea.

“Kwa mfano, mzazi au mwalimu anaweza kumwambia mtoto kuwa makosa ni sehemu ya kujifunza na mafanikio yanapatikana kwa kufanya mazoezi. Hili litawapa wanafunzi ujasiri wa kukabiliana na changamoto za somo hili bila woga,” anasema Mwalimu Veronica. 

Pia wape watoto changamoto ndogo ndogo wanazoweza kuzitatua kwa urahisi. Hii itawasaidia kuona hisabati sio somo gumu kama wanavyodhani au kuaminishwa. 

Mtaalam huyo wa hesabu anawashauri walimu wanaofundisha somo hilo kutumia mbinu za kisaikolojia zinazosaidia kujenga ujasiri wa wanafunzi. 

Mbinu rahisi kama kuanzisha maswali ya msingi, kuelezea dhana kwa njia ya mfano, na kuwapongeza kwa juhudi zao zinaweza kubadilisha mtazamo wao kuhusu hisabati.

Tumia mfano wa maisha halisi

Hisabati ipo kila mahali katika maisha yetu ya kila siku, na njia moja ya kumfanya mtoto aipende ni kuhusianisha somo hili na mazingira yanayomzunguka. 

Kwa mfano, mzazi anaweza kumwonyesha mtoto jinsi ya kuhesabu fedha anaponunua vitu dukani, kupanga bajeti ya matumizi ya nyumbani, au hata kupima vitu kama urefu na uzito.

Mfano mwingine ni michezo rahisi ya namba. Watoto wengi hupenda kucheza, na kwa kutumia michezo inayojumuisha hesabu, unaweza kuwafanya wajifunze kwa furaha.

Watoto wengi hupenda kucheza na kwa kutumia michezo inayojumuisha hesabu husaidia kuwajengea kumbukumbu nzuri kichwani. Picha/ Akili unde.

Hii huwasaidia kuelewa kuwa hisabati si somo la darasani tu bali ni ujuzi wa maisha ambao kila mtu anahitaji.

Pia katika shughuli za kila siku, mzazi anaweza kumuuliza mtoto maswali rahisi ya kihisabati kama, “tuna vijiko 10, tukiondoa viwili, vitabaki vingapi?”. 

Kwa njia hii, mtoto anapata fursa ya kujifunza hisabati kwa vitendo, jambo linalowafanya kuona somo hili kuwa la kufurahisha na linalotumika kila siku.

Nunua vitabu na programu za hisabati

Vitabu vya mazoezi ya hisabati ni nyenzo muhimu ya kujifunza, hasa kwa watoto wanaopenda kujifunza wakiwa nyumbani. 

Vitabu hivi vina maswali ya ngazi mbalimbali, kuanzia maswali rahisi hadi magumu, ambayo yanaweza kumsaidia mtoto kukuza maarifa yake hatua kwa hatua. 

Kwa mfano, vitabu vya watoto wa shule za msingi vinaweza kuwa na michoro na mifano ya kuvutia inayorahisisha uelewa wa dhana za msingi.

Uwepo wa vitabu mbalimbali humsaidia mtoto kuwa na uwezo wa kufanya maswali mengi kutoka kwenye vitabu tofauti. Picha/ Canva.

Kwa upande wa teknolojia, mzazi anaweza kutumia simu janja au kompyuta kuhamasisha mtoto kujifunza kupitia programu za kielimu.

Kuna programu nyingi za bure zinazopatikana mtandaoni ambazo zina michezo na maswali yanayofundisha hisabati kwa njia za kuvutia. 

Michezo kama hii inachochea ubunifu na hamasa kwa watoto, kwani wanajifunza kwa kucheza badala ya kuhisi wanalazimishwa.

Mbali na teknolojia, wazazi wanaweza kutumia majukwaa kama YouTube ambapo walimu wa hisabati huchapisha video za elimu. 

Video hizi zinaweza kuwa msaada mkubwa kwa watoto wanaopenda kujifunza kwa njia ya kuona, na zinawapa nafasi ya kurudia masomo mara kadhaa hadi waelewe kikamilifu.

Toa zawadi kwa mtoto akifanya vizuri

Kwa mfano, mzazi anaweza kumwekea mtoto changamoto ndogo, kama kumaliza maswali 10 ya hisabati, na kumpa zawadi endapo atamaliza kwa usahihi. 

Kulinganana tovuti ya Mrs Mayers Leaning Lab, watoto wanahamasika zaidi wanapopewa zawadi au pongezi kwa juhudi zao. 

Zawadi hizi zinaweza kuwa za vifaa kama kalamu, daftari, au hata vitu vidogo wanavyopenda, au maneno ya kuwahamasisha kama “Umefanya vizuri sana leo.”

Hii huwafanya watoto kuona hisabati kama mchezo wa kufurahisha unaowapa zawadi badala ya mzigo wa kimasomo unaowakandamiza.

Zawadi ni kitu kinachopendwa na kila mtu hivyo kumpa mtoto zawadi baada ya kufanya vizuri itamfanya kuongeza jitihada zaidi. Picha/ Canva.

Zaidi ya hayo, zawadi hizi huchochea ushindani wa afya ya akili miongoni mwa wanafunzi wa darasa moja au familia moja. 

Watoto wanapojua kuwa juhudi zao zinathaminiwa, wanakuwa na hamu zaidi ya kujifunza na kushinda changamoto nyingine. Hii huwasaidia kujiamini zaidi na kuona hisabati kama somo linalowezekana.

Michezo ya hisabati

Michezo ya namba ni njia bora ya kuwafanya watoto kushiriki kikamilifu katika kujifunza hisabati. 

Kwa mfano, michezo kama sudoku, ‘bingo’ ya namba, au kutafuta mifumo ya namba husaidia watoto kuboresha uwezo wao wa kufikiri.

Wakati wa kucheza, mzazi au mwalimu anaweza kuelezea dhana za hisabati zinazojitokeza kwenye mchezo husika, kama vile kujumlisha, kutoa, kuzidisha, au kugawanya.

Kwa kutumia michezo mbalimbali kunaweza kumsaidia mtoto kuwa na kumbukumbu za muda mrefu. Picha/ Canva.

Hii huwafanya watoto kuelewa kuwa hisabati si tu namba za kubahatisha bali ni somo linalohitaji mbinu na mikakati.

Michezo inayohusisha mashindano huwafanya watoto kuwa na hamu zaidi ya kushiriki. Wanafurahia changamoto wanapojaribu kuwashinda wenzao, huku wakiwa wanajifunza hisabati kwa vitendo. Kwa njia hii, hisabati inakuwa somo la kufurahisha na linalochochea maarifa mapya.

Tumia vifaa vya kuonyesha na vitu halisi

Watoto huelewa vizuri zaidi wanapofundishwa kwa kuona vitu halisi. Kwa mfano, walimu na wazazi wanaweza kutumia maharage, sarafu, au vijiti vya plastiki kufundisha dhana kama kuhesabu, kujumlisha, au kugawanya.

Mbali na vitu vya asili, chati na michoro pia ni nyenzo bora za kufundishia. 

Hii huwafanya watoto kuelewa dhana ngumu kwa urahisi zaidi ukilinganisha na njia za kawaida. Picha/ Canva.

Chati zinaweza kusaidia kuelezea mifumo ya namba, kama vile jedwali la kuzidisha, huku michoro ikielezea dhana za kijiometri kama pembe, mistari, na maumbo. Hii huwafanya watoto kuelewa dhana ngumu kwa urahisi zaidi.

Hii itawasaidia watoto kufikiri kuwa hisabati ni somo la vitendo na siyo nadharia pekee.

Anzisha mashindano ya hisabati

Mashindano ya hisabati ni njia nzuri ya kuwafanya watoto kujifunza kwa njia ya ushindani. 

Mashindano haya huwapa watoto nafasi ya kuonyesha maarifa yao, kujifunza kutoka kwa wenzao, na kupata hamasa ya kushinda zawadi au kutambuliwa.

Kwa mfano, kuna mashindano ya hisabati yanayoandaliwa na shule, vyuo, au taasisi za elimu, ambapo wanafunzi hushindana kutatua maswali ya hesabu kwa muda mfupi. Watoto wanaposhiriki katika mashindano haya, wanajifunza kushughulikia changamoto kwa haraka na kwa usahihi.

Kwenye mashindano siku zote kila mtu huwa na shauku ya kushinda hivyo na kwa watoto ushindani huwapa hamu ya kuwa bora zaidi. Picha/ Canva.

Kupitia mashindano haya, watoto hupata uzoefu wa kushirikiana na wenzao, jambo linalowasaidia kuboresha ujuzi wa kijamii na kuimarisha hamasa yao ya kujifunza. 

Wazazi wanashauriwa kuwatafutia watoto wao mashindano yanayofaa kulingana na umri na uwezo wao.

Elezea umuhimu wa hisabati katika maisha

Watoto mara nyingi huona hisabati kama somo lisilo na faida ya moja kwa moja katika maisha yao ya kila siku. 

Kwa kubadilisha mtazamo huu, mzazi au mwalimu anaweza kuwaonyesha umuhimu wa hisabati kwa kuelezea jinsi inavyotumika katika kazi mbalimbali kama biashara, uhandisi, sayansi, na hata burudani.

Kwa mfano, msanii wa muziki anahitaji hisabati ili kupanga bajeti ya muziki wake, huku mwanamichezo akitumia hisabati kupima muda na umbali wa mazoezi yake. 

Ni vyema kuwajengea uwezo wa kujitambua mapema watoto ili kadri wanavyokuwa wasione hesabu kama janga la Taifa. Picha/ Akili Unde.

Hii inawafanya watoto kuona hisabati kama nyenzo ya kufanikisha ndoto zao za maisha.

Kuelezea jinsi hisabati inavyotumika kusimamia fedha, kupanga ratiba, au hata kupima afya kunawapa watoto mtazamo wa kivitendo kuhusu somo hili. 

Matokeo yake ni kwamba wanajifunza kuipenda hisabati kwa sababu wanaona thamani yake katika maisha yao ya kila siku.

Kwa kutumia mbinu hizi, mzazi au mwalimu anaweza kubadilisha mtazamo wa mtoto kuhusu hisabati na kumfanya aipende na kuimudu kwa urahisi.

Undani idadi ya watalii wa kigeni ndani ya miaka 10 Tanzania

Katika kipindi cha miaka 10, Tanzania imepokea jumla ya watalii wa kigeni 13,711,190, ikiimarisha nafasi yake kama moja ya vivutio vikuu vya utalii barani Afrika. Mwaka 2024 umeibuka kuwa wenye mafanikio makubwa zaidi kwa sekta ya utalii, ukivutia watalii 2,141,895, idadi kubwa zaidi katika muongo mmoja.

Kwa upande mwingine, mwaka 2020 uliathirika pakubwa na janga la Uviko-19, ukirekodi idadi ndogo zaidi ya watalii 620,867. Hii inamaanisha kuwa idadi ya watalii walioingia mwaka 2024 ni mara tatu zaidi ya ile ya mwaka 2020, sawa na ongezeko la asilimia 244.9.

Mfumuko huu wa watalii unaonyesha mwelekeo mzuri wa sekta ya utalii, ambayo ina mchango mkubwa katika uchumi wa Taifa kwa kuongeza fedha za kigeni, fursa za ajira, na ukuaji wa biashara za ndani. Tanzania inaendelea kunufaika na vivutio vyake vya kipekee kama Hifadhi ya Serengeti, Mlima Kilimanjaro, Kreta ya Ngorongoro, na fukwe za Zanzibar.

Idadi ya watalii wa kigeni yapaa Tanzania

Tanzania imeendelea kung’ara katika sekta ya utalii baada ya kurekodi ongezeko kubwa la idadi ya watalii wa kigeni mwaka 2024. Kwa mujibu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), jumla ya watalii 2,141,895 waliingia nchini, ikiwa ni ongezeko la asilimia 18.58 ikilinganishwa na mwaka 2023.

Hii ni mara tatu zaidi ya idadi ya watalii walioingia nchini mwaka 2020 wakati dunia ilipokumbwa na janga la Uviko-19, ambapo ni 620,867 pekee waliotembelea Tanzania.

Kwa upande wa miezi, Julai umeibuka kinara kwa kuvutia wageni wengi zaidi, huku watalii 218,065 wakiwasili nchini. Kinyume chake, Aprili ndiyo ilikuwa na idadi ndogo zaidi, ikiwa na watalii 116,280 pekee.

Ongezeko hili linaonyesha mvuto wa Tanzania kama kivutio cha utalii duniani, huku vivutio kama Hifadhi ya Serengeti, Mlima Kilimanjaro, na fukwe za Zanzibar vikichangia kwa kiasi kikubwa.

Nchi 10 Afrika zilizopokea msaada mkubwa sekta ya afya kutoka USAID 2023

Kwa miaka mingi, Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID) limekuwa msaada wa huduma za afya barani Afrika, likifadhili mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI, kifua kikuu, magonjwa ya mlipuko, na kuboresha mifumo ya afya. 

Kwa mujibu wa Shirika la Misaada la Serikali la Marekani (Foreign Assistant Government) nchi 10 zilizonufaika zaidi kwa mwaka 2023 ni Kenya, Nigeria, Tanzania, Uganda, Ethiopia, Msumbiji, Zambia, Afrika Kusini, Malawi, na DRC, ambapo misaada hii imewezesha upatikanaji wa dawa, vifaa tiba, lishe bora, na huduma za afya ya uzazi.

Tanzania ni nchi iliyoongoza kwa kupokea msaada mkubwa katika sekta ya afya kutoka USAID ikipokea takriban Dola milioni 512.8 za Marekani, sawa na Sh1.32 trilioni.

Hata hivyo, kusitishwa kwa misaada hii kunaweza kuwa na athari kubwa katika nchi hizi kwa kukabiliwa na uhaba wa dawa za Virusi vya Ukimwi (VVU) na Upungufu wa Kinga Mwilini (UKIMWI), lishe, kifua kikuu, magonjwa ya mlipuko na vitisho vipya vya kiafya, vifaa vya afya, uzazi wa mpango na afya ya uzazi, usafi wa maji, pamoja na miradi mingine ya afya.

Bila ufadhili wa USAID, nchi hizi zinapaswa kutafuta vyanzo mbadala vya rasilimali ili kuzuia madhara kwa mamilioni ya watu wanaotegemea huduma hizi. Lakini je, mataifa haya yana uwezo wa kuziba pengo hili haraka? Ikiwa suluhisho halitapatikana, mustakabali wa afya barani Afrika unaweza kuwa hatarini.

Tumbaku yazitikisa kahawa, korosho mauzo nje ya nchi Tanzania

  • Thamani ya mauzo nje ya nchi yaongezeka takriban mara mbili ndani ya mwaka mmoja.

Dar es Salaam. Tumbaku ni moja ya bidhaa tatu asilia zinazoongoza kwa kuuzwa kwa wingi nje ya Tanzania na zilizoingiza fedha nyingi za kigeni licha ya kupigwa vita na wadau wa afya kuwa inahatarisha maisha ya watumiaji. 

Kwa mujibu wa Ripoti ya Hali ya Uchumi Tanzania mwaka 2023 iliyotolewa na Wizara ya Fedha hivi karibuni, katika bidhaa za asilia zinazouzwa nje ya nchi tumbaku inachuana kwa mbali na kahawa na korosho. 

Korosho, kahawa, chai na mkonge ni miongoni mwa mazao makubwa ya asilia ambayo huchangia kwa kiwango kikubwa fedha za kigeni nchini ila ukuaji wa uzalishaji wa tumbaku umezidi kuyapiga kikumbo mazao hayo. 

“Mwaka 2023, thamani ya mauzo ya tumbaku nje ilikuwa Dola za Marekani milioni 340.4 (Sh828.2 bilioni) ikilinganishwa na Dola za Marekani milioni 178.5 (Sh411.5 bilioni) mwaka 2022, sawa na ongezeko la asilimia 90.7,” inasema ripoti hiyo iliyotolewa na Wizara ya Fedha.

Ripoti hiyo inaeleza kuwa mafanikio hayo yalitokana na kuongezeka kwa mauzo ya tumbaku kwa zaidi ya mara moja na nusu hadi kufikia tani 82,000 mwaka 2023 kutoka tani 49,300 mwaka 2022. 

Uuzaji wa zao hilo nje ya nchi ulienda sanjari na kiwango cha uzalishaji wa tumbaku ulioongezeka takriban mara mbili ndani ya mwaka mmoja kutoka tani 70,699 mwaka 2022 hadi tani 122,859 mwaka jana. 

Uzalishaji wa tumbaku umekuwa ukiongezeka mwaka hadi mwaka Tanzania jambo lililochochea ongezeko la kiwango cha zao hilo kuuzwa nje ya nchi. Picha: Akili Mnemba. Picha hii imetengenezwa na akili mnemba kwa ajili ya kuongeza muktadha kwenye makala hii tu na si kuonyesha uhalisia.

Bei yaibeba tumbaku

Wastani wa bei ya kuuza tumbaku uliongezeka kwa asilimia 14.5 katika soko la dunia na kufikia Dola za Marekani 4,150.8 (Sh11.1 milioni) kwa tani mwaka 2023 kutoka Dola za Marekani 3,624.1(Sh9.7 milioni) kwa tani mwaka 2022.

Ingawa kiasi cha wingi wa korosho kinachouzwa nje ya Tanzania ni zaidi ya mara mbili ya kiasi cha tumbaku na kahawa, thamani ya tumbaku kwenye soko la kimataifa inazidi kwa zaidi ya mara 1.5 ya thamani ya korosho na kahawa. 

Kwa hesabu hizo, tumbaku inakuwa bidhaa asilia yenye thamani kubwa zaidi inayouzwa nje ya nchi. Bidhaa nyingine zisizoasilia zinazochangia zaidi fedha za kigeni ni dhahabu, utalii na bidhaa za viwandani. 

Miaka ya hivi karibuni kumekuwa na hamasa kubwa ya kuongeza ufanisi katika uzalishaji wa tumbaku kwa kutumia mbinu za kisasa za kilimo na kuimarisha uchakataji wake ili kupunguza athari kwa mazingira.

Mfano, kampuni Mkwawa Tobacco Processing Limited (MTPL), imeendelea kufanya uwekezaji mkubwa katika usindikaji tumbaku, ikiongeza ajira na kuinua uchumi wa wananchi na wafanyabiashara. 

Uwekezaji huo katika uzalishaji na usindikaji unaofanywa na wakulima na viwanda vya zao hilo, unafanya tumbaku kuwa ni miongoni mwa bidhaa asilia zinazochangia kiwango kikubwa kwenye pato la taifa.  

Pamoja na uwekezaji huo kumekuwa na presha kubwa kutoka kwa wadau wa afya hasa wanaharakati wakiitaka Serikali kudhibiti vikali uzalishaji na utumiaji wa tumbaku unaochangia maradhi kwa binadamu ikiwemo matatizo ya mapafu.

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...

Enable Notifications OK No thanks