Fursa, watumiaji wa intaneti Tanzania wakifikia milioni 58.1

  • Hadi kufikia robo ya mwaka inayoishia Desemba 2025, watumiaji wa intaneti walikuwa milion 58.1 kutoka milioni 56.3 iliyorekodiwa Septemba 2025.
  • Intaneti hiyo hutumiwa zaidi na simu za janja. 
  • Hiyo inaongeza idadi ya Watanzania wanaonufaika na fursa za mtandaoni. 

Dar es Salaam. Idadi ya Watanzania wanaotumia huduma za intaneti imeendelea kuongezeka kwa kasi na kufikia milioni 58.1 suala linalotajwa kuendelea kufungua fursa zaidi za kiuchumi.

Takwimu za mawasiliano za robo ya nne ya mwaka 2025 zilizotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) zinaonesha matumizi ya huduma z aintaneti yameongezeka kwa asilimia 3.2.

Takwimu hizo zinaonyesha kuwa hadi kufikia Desemba 2025 watumiaji wa intaneti walifikia milioni 58.1 kutoka watumiaji  56.3 waliokuwepo Septemba 2025.

Idadi hiyo ni sawa na ongezeko la watumiaji milioni 1.8 ndani ya kipindi cha miezi mitatu kuanzia Septemba hadi Disemba mwaka jana.

Kwa mujibu wa TCRA, idadi hiyo inajumuisha laini zote zilizotumia huduma ya intaneti angalau mara moja katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita, bila kujali teknolojia iliyotumika kupitia njia mbalimbali, zikiwemo laini za simu za mkononi, nyaya za faiba (fiber), pamoja na teknolojia za mawimbi (wireless). 

Uchambuzi wa takwimu hizo uliofanywa na Nukta Habari kwa miaka 10 mfululizo umebaini ongezeko la watumiaji wa intaneti nchini Tanzania mwaka hadi mwaka.

Huenda ukuaji huo umechangiwa kwa kiasi kikubwa na kuendelea kuimarika kwa miundombinu ya mawasiliano nchini, ikiwemo ongezeko la minara ya simu iliyofikia 10,029 kufikia mwisho wa mwaka 2024.

Aidha, intaneti inayotumia mtandao wa simu za mkononi (mobile wireless internet) imeendelea kuwa njia kuu ya upatikanaji wa huduma hiyo, ikichangia asilimia 99 ya usajili wote wa intaneti nchini. 

Mbali na ongezeko la matumizi ya intaneti, matumizi ya simu janja (smartphones) pia yameongezeka, ambapo kiwango cha upenyo wake kimefikia asilimia 41.82. 

Hata hivyo, simu za kawaida (feature phones) bado zinaendelea kutumika kwa kiwango kikubwa zaidi zikiwa na asilimia 87.11 ya matumizi.

Ni fursa iliyojificha

Wachambuzi wa uchumi wanaeleza kuwa ongezeko hilo la matumizi ya intaneti linafungua fursa mpya katika biashara, elimu, huduma za kifedha na ajira za kidijitali, huku likichochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali nchini.

Akizungumza kuhusu mwenendo huo, Profesa Abel Kinyondo wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) amesema kuwa ongezeko la usajili wa laini zinazotumia intaneti halimaanishi moja kwa moja kuwa idadi hiyo ni sawa na watumiaji halisi, kwa kuwa mtu mmoja anaweza kuwa na laini zaidi ya moja.

Amefafanua kuwa pamoja na changamoto zilizopo, intaneti imeleta mapinduzi makubwa katika shughuli za kiuchumi kwa kurahisisha biashara, masoko na huduma za kifedha.

“Leo mtu anaweza kufanya biashara akiwa sehemu yoyote nchini bila kulazimika kusafiri. Intaneti imeongeza urahisi wa kufanya miamala, kutangaza bidhaa na kupata taarifa mbalimbali kwa haraka,” amesema Profesa Kinyondo.

Hata hivyo, ameonya kuwa matumizi ya intaneti yanaambatana na changamoto mbalimbali zikiwemo uhalifu wa mtandaoni, udanganyifu katika biashara za mtandaoni na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii.

Pia amewataka vijana kutumia intaneti kwa manufaa, ikiwemo kujifunza ujuzi mpya, kufanya biashara na kutafuta maarifa, huku wakizingatia tahadhari dhidi ya matumizi yanayoweza kuhatarisha usalama wao binafsi na maadili ya jamii.

Idadi ya redio yazidi kupaa Tanzania

  • Idadi ya vituo vya redio Tanzania imezidi kuongezeka kwa kasi baada ya vituo 17 kuanzishwa ndani ya mwaka mmoja.

Dar es Salaam. Wakati dunia ikiadhimisha Siku ya Redio leo Februari 13, 2022, redio ni chombo muhimu ambacho Watanzania wana kitumia kupata habari zinazowawezesha kufanya maamuzi katika maisha yao ya kila siku.

Licha ya kuongezeka kwa changamoto za kifedha zinazoendelea kuvikabili vyombo mbalimbali vya habari duniani, idadi ya vituo vya redio Tanzania imezidi kuongezeka kwa kasi baada ya vituo 17 kuanzishwa ndani ya mwaka mmoja.

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inaeleza katika ripoti mpya ya mawasilino ya robo ya mwisho ya mwaka 2021 kuwa hadi Desemba mwaka jana kulikuwa na vituo 210 vya redio nchini kutoka vituo 193 mwaka 2020.

Uchambuzi wa mwenendo wa takwimu za vituo vya redio uliofanywa na Nukta (www.nukta.co.tz) unaonyesha kuwa vituo vingi vya redio vilizaliwa mwaka 2016 baada ya vituo 42 kuanzishwa ndani ya mwaka mmoja.

Hata hivyo, mwaka 2018 ndiyo mwaka ambao vituo vichache zaidi vilianzishwa ndani ya mwaka mmoja kutokana na kuongezeka kwa vituo viwili tu vya redio kutoka 156 mwaka 2017 hadi 158 mwaka 2018.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Nukta TV

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Nukta TV

Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV