Necta yatangaza matokeo ya kidato cha nne 2025 ufaulu waongezeka kwa asilimia 2.61
January 31, 2026 11:30 am ·
Lucy Samson
Arusha. Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya mitihani ya kidato cha nne iliyofanyika Novemba, 2025, ambapo ufaulu umeongezeka kiduchu.
Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Dk. Said Mohamed aliyekuwa akitangaza matokeo hayo jijini Dar es Salaam leo Januari 31, 2026 amesema kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia 2.61 kulinganisha na ufaulu wa mwaka 2024.
“Takwimu zinaonesha kuwa ufaulu wa jumla umepanda kwa asilimia 2.61 na hivyo kufikia asilimia 94.98 ambapo watahiniwa 526,620 wamefaulu kwa kupata dvision I, II, III, na IV, mwaka 2024 watahiniwa waliofaulu walikuwa 477,262 sawa na asilimia 92.37 na mwaka 2023 walikuwa 471,427 sawa na asilimia 89.36 ,” amesema Dk Said.
Latest
20 hours ago
·
Fatuma Hussein
BoT: Dhahabu itakayouzwa haitatumika kugharamia miundombinu Tanzania
21 hours ago
·
Kelvin Makwinya
Serikali, NMB kushirikiana kutoa mikopo nafuu kuinua wajasiriamali wadogo
22 hours ago
·
Mwandishi
Tanzania yazindua mfuko wa Sh2 bilioni kusaidia watengeneza maudhui
1 day ago
·
Kelvin Makwinya
Viwango vya kubadili fedha Januari 30, 2026