Necta yatangaza matokeo ya kidato cha nne 2025

January 31, 2026 11:30 am · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Watahiniwa 526,620 wamefaulu kwa kupata dvision I, II, III, na IV.

Arusha. Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya mitihani ya kidato cha nne iliyofanyika Novemba, 2025, ambapo ufaulu umeongezeka kiduchu.

Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Prof Said Mohamed aliyekuwa akitangaza matokeo hayo jijini Dar es Salaam leo Januari 31, 2026 amesema kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia 2.61 kulinganisha na ufaulu wa mwaka 2024.

“Takwimu zinaonesha kuwa ufaulu wa jumla umepanda kwa asilimia 2.61 na hivyo kufikia asilimia 94.98 ambapo watahiniwa 526,620 wamefaulu kwa kupata dvision I, II, III, na IV, mwaka 2024 watahiniwa waliofaulu walikuwa 477,262 sawa na asilimia 92.37 na mwaka 2023 walikuwa 471,427 sawa na asilimia 89.36 ,” amesema Prof Said.

Kwa mujibu wa Necta, jumla ya watahiniwa wa shule 595,810 walisajiliwa kufanya mtihani huo ambapo asilimia 97.49 sawa na watahiniwa 555,606 walijitokeza kufanya mitihani hiyo Novemba 10 hadi 28 mwaka 2025.
Watahiniwa 14,277 sawa na asilimia 2.51 hawakufanya mtihani huo kutokana na sababu mbalimbali licha ya kuwa walisajiliwa.


Ubora wa ufaulu waongezeka
Dk Said amewaambia wanahabari kuwa ubora wa ufaulu kwa mwaka 2025 umeongezeka kwa asilimia 3.1 kulinganisha na ule wa mwaka 2024.


Ubora wa ufaulu hupimwa kwa kuangalia idadi ya wanafunzi waliopata daraja la kwanza hadi la tatu ambapo kwa mwaka 2025 watahiniwa 255,404 sawa na asilimia 46 walipata madaraja hayo.


Mwaka 2024 watahiniwa waliopata ufaulu wa Madaraja ya I III walikuwa 221,953 sawa na asilimia 42.96.


Kwa mujibu wa Necta katika kipengele cha ubora wa ufaulu wavulana wamefanya vizuri zaidi kulinganisha wasichana.


“…Wavulana ni 135,676 sawa na asilimia 52.30 ya Wavulana wote wenye matokeo na Wasichana ni 119,728 sawa na asilimia 40.58 ya Wasichana wote wenye matokeo.,”amesema Prof Said.

/
No matches found for this filter
22 May, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
23 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
23 May, 2026
No active movers today
Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MIKOA YA KIPOLISI ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI TANZANIA BARA 2025

MIKOA YA KIPOLISI ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI TANZANIA BARA 2025

Nukta TV

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

Nukta TV

MIKOA 5 ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI 2025 TANZANIA BARA

MIKOA 5 ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI 2025 TANZANIA BARA

Nukta TV