Maspika wa Bunge la Tanzania tangu uhuru

November 10, 2025 6:21 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Tangu kupatikana kwa uhuru mwaka 1961, Tanzania imepata viongozi kadhaa waliowahi kushika nafasi ya Spika wa Bunge. Spika wa kwanza alikuwa A.Y.A. Karimjee, aliyeliongoza Bunge la Tanganyika kuanzia mwaka 1956 hadi 1962. 

Baada ya hapo, nafasi hiyo ilishikiliwa na Chief Adam Sapi Mkwawa, ambaye alihudumu kwa kipindi kirefu zaidi kuanzia mwaka 1962 hadi 1973, na tena kati ya mwaka 1975 hadi 1994.

Chief Erasto Mang’enya aliongoza kwa muda mfupi kati ya mwaka 1973 na 1975, kabla ya Pius Msekwa kuchukua nafasi hiyo mwaka 1994 na kuhudumu hadi 2005. 

Wengine waliowahi kushika nafasi hiyo ni Samuel Sitta (2005–2010), Anne Makinda (2010–2015), Job Ndugai (2015–2022), na kwa sasa Dk. Tulia Ackson, ambaye alianza Februari 2022 na ambaye ukomo wake unakwenda kufikia Novemba 11, 2025 atakapa chaguliwa Spika mpya.

Kwa zaidi ya nusu karne, Bunge limepitia mabadiliko makubwa ya kisiasa na kiutendaji chini ya uongozi wa maspika hao. Hata hivyo, swali linaloibuka sasa ni, nani atarithi mikoba ya Dk. Tulia Ackson na kuwa Spika wa Bunge la 13 la Tanzania?

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV