Maspika wa Bunge la Tanzania tangu uhuru

November 10, 2025 6:21 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Tangu kupatikana kwa uhuru mwaka 1961, Tanzania imepata viongozi kadhaa waliowahi kushika nafasi ya Spika wa Bunge. Spika wa kwanza alikuwa A.Y.A. Karimjee, aliyeliongoza Bunge la Tanganyika kuanzia mwaka 1956 hadi 1962. 

Baada ya hapo, nafasi hiyo ilishikiliwa na Chief Adam Sapi Mkwawa, ambaye alihudumu kwa kipindi kirefu zaidi kuanzia mwaka 1962 hadi 1973, na tena kati ya mwaka 1975 hadi 1994.

Chief Erasto Mang’enya aliongoza kwa muda mfupi kati ya mwaka 1973 na 1975, kabla ya Pius Msekwa kuchukua nafasi hiyo mwaka 1994 na kuhudumu hadi 2005. 

Wengine waliowahi kushika nafasi hiyo ni Samuel Sitta (2005–2010), Anne Makinda (2010–2015), Job Ndugai (2015–2022), na kwa sasa Dk. Tulia Ackson, ambaye alianza Februari 2022 na ambaye ukomo wake unakwenda kufikia Novemba 11, 2025 atakapa chaguliwa Spika mpya.

Kwa zaidi ya nusu karne, Bunge limepitia mabadiliko makubwa ya kisiasa na kiutendaji chini ya uongozi wa maspika hao. Hata hivyo, swali linaloibuka sasa ni, nani atarithi mikoba ya Dk. Tulia Ackson na kuwa Spika wa Bunge la 13 la Tanzania?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...

Enable Notifications OK No thanks