Ufaulu kidato cha nne unavyopanda na kushuka Tanzania

January 31, 2026 3:00 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Takwimu zinaonesha ufaulu unashuka na kuongezeka  mwaka hadi mwaka katika kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka 2021.

Dar es Salaam. Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya mitihani ya kidato cha nne iliyofanyika Novemba, 2025, ambapo ufaulu umeongezeka kidogo kulinganisha na miaka iliyopita.

Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Dk. Said Mohamed aliyekuwa akitangaza matokeo hayo jijini Dar es Salaam leo Januari 31, 2026 amesema kuwa ufaulu wa wanafunzi kwa kidato cha nne kwa mwaka 2025 ni asilimia 92.37. 

Uchambuzi uliofanywa na Nukta Habari unaonyesha kuwa ufaulu wa kidato cha nne umekuwa ukipanda na kushuka kwa miaka tofauti katika kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka 2021.

Takwimu zinaonyesha kiwango cha ufaulu kiliongezeka kwa asilimia 0.67 na kufikia asilimia 87.79 mwaka 2022 kutoka asilimia 87.30 iliyorekodiwa mwaka 2021. Hata hivyo, ufaulu huo ulishuka kwa asilimia 0.32 na kufikia asilimia 87.65 mwaka 2023.

Ongezeko thabiti la matokeo ya kidato cha nne limeonekana kuanzia mwaka 2024 ambapo ufaulu uliongezeka kwa takriban asilimia 4.72 na kufikia asilimia 92.37.

Aidha, katika kipindi cha miaka mitano wavulana ndio wanaongoza kwa kuwa na ufaulu wa juu zaidi ya wasichana wakiwa na wastani wa ufaulu wa asilimia 92.75 wakiwaacha mbali wasichana wenye wastani wa asilimia 90.71.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...

Enable Notifications OK No thanks