Tanzania kinara idadi ya Simba Afrika

January 12, 2026 1:34 pm · Goodluck Gustaph
Share
Tweet
Copy Link

Shirika la World Population Review limeitaja Tanzania kuwa na simba 14,500 idadi inayoifanya kuwa kinara wa idadi kubwa ya Simba barani Afrika.

Katika mbuga zake za kitaifa na mapori ya akiba nchini Tanzania, unaweza kuona simba jike wakiwinda alfajiri, madume wakinguruma na wengine wakiwinda au kupumzika katika vivuli vya miti.

Unaweza kujionea wanyama hao katika hifadhi mbalimbali ikiwemo Serengeti, Ngorongoro, Tarangire na Ruaha.

Hata hivyo, takwimu hizo zinatofautiana na zile zilizotolewa na IUCN pamoja na Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) ambao waliripoti idadi ya simba hao kuwa 17,000.

Nchi nyingine yenye idadi kubwa ya simba ni Afrika Kusini (Simba 3,284), Botswana (Simba 3,063), Kenya (Simba 2,515) na Zambia (Simba 2,500)

Pamoja na hayo, Tawiri ilibainisha kuwa Tanzania imeongoza barani Afrika kwa kuwa na idadi kubwa ya wanyama wengine ikiwemo Nyati na Chui.


Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia kuendeleza fursa za ajira nje ya nchi, Rais Mwinyi akiongeza kima cha mshahara Zanzibar.

Rais Samia kuendeleza fursa za ajira nje ya nchi, Rais Mwinyi akiongeza kima cha mshahara Zanzibar.

Nukta TV

RAIS SAMIA: Hakuna ustawi wa mfanyakazi bila utulivu wa Taifa

RAIS SAMIA: Hakuna ustawi wa mfanyakazi bila utulivu wa Taifa

Nukta TV

RAIS SAMIA: Serikali itaendelea kuboresha masilahi ya watumishi kadri uchumi utakavyoruhusu

RAIS SAMIA: Serikali itaendelea kuboresha masilahi ya watumishi kadri uchumi utakavyoruhusu

Nukta TV