Tanzania kinara idadi ya Simba Afrika

January 12, 2026 1:34 pm · Goodluck Gustaph
Share
Tweet
Copy Link

Shirika la World Population Review limeitaja Tanzania kuwa na simba 14,500 idadi inayoifanya kuwa kinara wa idadi kubwa ya Simba barani Afrika.

Katika mbuga zake za kitaifa na mapori ya akiba nchini Tanzania, unaweza kuona simba jike wakiwinda alfajiri, madume wakinguruma na wengine wakiwinda au kupumzika katika vivuli vya miti.

Unaweza kujionea wanyama hao katika hifadhi mbalimbali ikiwemo Serengeti, Ngorongoro, Tarangire na Ruaha.

Hata hivyo, takwimu hizo zinatofautiana na zile zilizotolewa na IUCN pamoja na Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) ambao waliripoti idadi ya simba hao kuwa 17,000.

Nchi nyingine yenye idadi kubwa ya simba ni Afrika Kusini (Simba 3,284), Botswana (Simba 3,063), Kenya (Simba 2,515) na Zambia (Simba 2,500)

Pamoja na hayo, Tawiri ilibainisha kuwa Tanzania imeongoza barani Afrika kwa kuwa na idadi kubwa ya wanyama wengine ikiwemo Nyati na Chui.


Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
WAMESANUKA, mbinu mpya ya usafirishaji wa dawa za kulevya yafichuliwa

WAMESANUKA, mbinu mpya ya usafirishaji wa dawa za kulevya yafichuliwa

Nukta TV

CCM yatoa ratiba maombi ya kumrithi Lukuvi, Israel, Lebanon wakisitisha mapigano

CCM yatoa ratiba maombi ya kumrithi Lukuvi, Israel, Lebanon wakisitisha mapigano

Nukta TV

Ridhiwani: Serikali inalenga kuacha tabasamu kwa watumishi wa Umma

Ridhiwani: Serikali inalenga kuacha tabasamu kwa watumishi wa Umma

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.