Ufaulu wa hisabati darasa la nne waimarika

January 12, 2026 2:31 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam.Ufaulu wa somo la hisabati kwa wanafunzi wa darasa la nne umeendelea kuimarika kwa miaka mitatu mfululizo suala linalotoa muelekeo chanya wa ubora wa elimu ya msingi nchini.

Kwa mujibu wa matokeo ya darasa la nne yaliyotangazwa na Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) Januari 10, 2026, asilimia 81.44 ya wanafunzi waliofanya mitihani wa hesabu mwaka 2025 wamefaulu.

“ “Somo la hisabati limeendelea kuimarika kwa ngazi ya darasa la nne kwani wanafunzi waliopata daraja E wamepungua kwa asilimia 10 na waliofaulu kwa daraja A wameongezeka kwa asilimia 10,” inaeleza taarifa ya Prof Mohamed.

Kwa takwimu hizo ni sawa na kusema wanafunzi 1,490,377 kati ya wanafunzi 1,583,686 walofanya mitihani hiyo Oktoba 22 na 23, mwaka 2025 wamefaulu.

Kutokana na ufaulu huo wanafunzi 8 kati ya kila 10 waliofanya mitihani hiyo  wamefaulu somo la hisabati, suala linalotoa ahueni kwa walimu na wazazi ambao miaka ya nyuma walikuwa wakosota kutafuta suluhu ya kupandisha ufaulu wa somo hilo.

Kwa mujibu wa Necta, ufaulu huu wa mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 10.04 ukilinganisha na ufaulu wa mwaka 2024 ambao ulikuwa asilimia 71.4 huku mwaka 2023 ufaulu ukikuwa asilimia 54.

Hii inaashiria ongezeko la takribani asilimia 27 ndani ya kipindi cha miaka miwili, jambo linaloonyesha muelekeo chanya wa elimu ya msingi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV