Nchi za Afrika zinazoongoza utoaji chanjo ya Uviko-19

August 28, 2021 12:29 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Orodha inaongozwa na Afrika Kusini ambayo imetoa dozi zaidi ya milioni 9 kwa raia wake.
  • Nchi nyingine ni pamoja na Kenya, Ethiopia na Nigeria.
  • Hadi sasa Tanzania haijafikisha watu 500,000 waliopata chanjo.

Dar es Salaam. Licha ya baadhi ya watu kuwa na mashaka juu ya chanjo ya ugonjwa wa Corona (Uviko-19), wapo waliokubali kupata chanjo hiyo ili kuepuka madhara yatokanayo na ugonjwa huo.

Waziri wa Afya Dk Gwajima mwishoni mwa mwezi Julai alisema, kupata chanjo ya Corona kutamsaidia mtu kutokufikia hatua ya kulazwa hata atakapopata ugonjwa huo.

Kwa dunia, takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonyesha kuwa takriban dozi bilioni 5 za chanjo ya Uviko-19 zimetolewa duniani na watu bilioni 1.1 duniani wamepata dozi kamili ya chanjo dhidi ya ugonjwa huo

Zipo chanjo zinazotolewa kwa dozi mbili kama Pfizer na Moderna na zinazotolewa kwa dozi moja ikiwemo Johnson & Johnson ambayo pia inatolewa nchini Tanzania.

Kwa Tanzania, WHO inaeleza kuwa dozi 218,621 za chanjo ya Corona zimetolewa ikiwa zoezi la chanjo nchini lilianza mwishoni mwa mwezi Julai.

Hata hivyo, kasi ya utoaji chanjo barani humo hairidhishi kwa sababu ni nchi nne tu katika 54 ambazo zimefanikiwa kuchanja zaidi ya asilimia 10 ya wa raia wake.

Katika video hii, utaona nchi ambazo zimetoa dozi nyingi zaidi za chanjo barani Afrika pamoja na aina ya chanjo zinazotolewa nchini humo:

                 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
6 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
6 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV