Mifugo ya nyumbani yaongezeka kwa zaidi ya asilimia 40 Tanzania
- Imeongeza hadi milioni 157.9 mwaka 2019/20 kutoka milioni 21.4 mwaka 2007/08.
- Zaidi ya nusu ya mifugo hiyo ni kuku.
- Ufugaji wa kienyeji na teknolojia duni kikwazo kwa wafugaji kunufaika.
Dar es Salaam. Huenda Watanzania wakafaidika na wanyama wa kufugwa nyumbani baada ya ripoti mpya kuonyesha kuwa idadi ya wanyama hao imeongezeka kwa asilimia 44.2 ndani ya miaka 10.
Wanyama wa kufugwa ambao hutumika kwa ajili kitoweo na shughuli za biashara hujumuisha mbuzi, ng’ombe, nguruwe, kuku na kondoo.
Ripoti ya Sampuli ya Sensa ya Kilimo kwa mwaka 2019/20 kuhusu mazao, sekta ya mifugo na ufugaji wa samaki iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) hivi karibuni inaeleza kuwa hadi kufikia Agosti 2020, Tanzania ilikuwa na wanyama wa kufugwa milioni 157.9.
Idadi hiyo imeongezeka kutoka wanyama milioni 88 waliorekodiwa mwaka 2007/08 ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 44.2 ndani ya miaka 10.
Sehemu kubwa ya mifugo hiyo inamilikiwa na wananchi wa kawaida ambao hufuga kienyeji kwa ajili kujipatia kipato cha kuendesha familia.Â
Ripoti hiyo inaonyesha, Watanzania wanafuga kwa wingi kuku kuliko wanyama wengine, ambapo hadi Agosti 2020 kulikuwa na kuku milioni 87.7 sawa na asilimia 55.5 ya wanyama wote wa kufugwa waliohusishwa katika sensa hiyo.Â
Kuku ambao huwa ni wa kisasa na kienyeji wamefuatiwa kwa mbali na ng’ombe ambao wamerekodiwa kufikia milioni 33.9.Â
Idadi ya ng’ombe imeongezeka kutoka milioni 21.4 waliokuwepo mwaka 2007/08, licha ya kuwa bado wafugaji hawajafaidika kikamilifu kutokana changamoto mbalimbali ikiwemo kufuga kienyeji na kutokuwa na teknolojia ya kisasa.Â
Tanzania ni nchi ya pili Afrika kwa kuwa na ng’ombe wengi baada ya Ethiopia ambayo ina ng’ombe zaidi ya milioni 60.Â

Latest