Shilingi yaimarika dhidi ya Euro na Pauni yabaki tulivu dhidi ya dola
- Wanunuzi wa sarafu hizo wataendelea kununua sarafu hiyo kwa bei nafuu huku wauzaji wakinufaika kwa kupata kiasi kikubwa cha shilingi.
Dar es Salaam. Shilingi ya Tanzania yaimarika dhidi ya Euro na Pauni ya Uingereza huku ikibaki tulivu dhidi ya Dola ya Marekani Agosti 14, 2026.
Kwa mujibu wa viwango vilivyo chapishwa na benki za NMB na CRDB zinaonyesha kuwa Dola ya Marekani imeendelea kuuzwa katika viwango sawa na jana katika benki zote mbili.
Hata hivyo, kwa upande wa Euro, benki ya CRDB imeshusha bei ya kununua na kuuza Euro kutoka Sh2,907.66 na Sh3,207.66 kwa Euro moja jana hadi Sh2,902.89 na Sh3,202.89 leo. Hii ni punguzo la Sh4.77 kwa kila Shilingi moja.
Kwa NMB Bank, Euro imeshuka kutoka Sh2,904 hadi Sh2,900 kwa bei ya kununua na kutoka Sh3,177 hadi Sh3,173 kwa bei ya kuuza.

Kwa Pauni ya Uingereza, CRDB imeshusha kiwango cha kununua kutoka Sh3,430.33 hadi Sh3,423.60, huku kiwango cha kuuza kikishuka kutoka Sh3,730.33 hadi Sh3,723.60. Hivyo, viwango vyote viwili vimepungua kwa Sh6.73.
Mabadiliko tofauti yameonekana NMB ambapo imeshusha bei ya kununua kutoka Sh3,371 hadi Sh3,365, lakini bei ya kuuza imeongezeka kutoka Sh3,717 hadi Sh3,741.
Kwa upande wa sarafu za kikanda viwango vya Shilingi ya Kenya na Shilingi ya Uganda katika CRDB pia imebaki katika viwango sawa na jana.