Viwango vya fedha za kigeni vinavyotumika CRDB, NMB leo
- Shilingi ya Tanzania yaendelea kuimarika dhidi ya Dola ya Marekani.
Dar es Salaam. Viwango vya kubadilisha fedha vilivyotolewa na Benki za CRDB na NMB leo Septemba 10, 2026 vinaonyesha tofauti katika bei za ununuzi na uuzaji wa sarafu mbalimbali dhidi ya Shilingi ya Tanzania.
Kwa mujibu wa viwango hivyo, Dola ya Marekani inanunuliwa leo kwa Sh2,600 na kuuzwa kwa Sh2,680 katika CRDB, wakati NMB ikinunua kwa Sh2,595 na kuuza kwa Sh2,675.
Pauni ya Uingereza (GBP) ina thamani ya juu zaidi, ambapo CRDB imenunua kwa Sh3,449.95 na kuuza kwa Sh3,779.95, huku NMB ikiwa na Sh3,560 kwa ununuzi na Sh3,714 kwa uuzaji.
Sarafu nyingine zilizo kwenye viwango hivyo licha ya kupanda na kushuka kwa baadhi ni Euro, Yuan ya China, Shilingi ya Kenya, Rand ya Afrika Kusini, Shilingi ya Uganda na Rupia ya India.
