BoT kuchukuliwa hatua wanaofanya biashara ya kukopesha bila leseni
- Wananchi watakiwa kuchukua tahadhari.
- Faini ya Sh20 milioni au kifungo cha miaka miwili kutolewa kwa watakaokaidi.
Dar es Salaam. Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imewataka Watanzania kuepuka kukopa au kufanya biashara na taasisi, kampuni au mtu binafsi ambao hawana leseni ili kuepuka kutapeliwa.
BoT imebaini kuwa kuna baadhi ya taasisi, kampuni na watu binafsi wanaojihusisha na biashara ya kutoa mikopo bila ya kuwa na leseni, jambo ambalo ni kinyume na sheria.
BOT imeyasema hayo kupitia taarifa yake iliyotolewa jana Novemba 24, 2022 na kusistiza hatua kali zitakazochukuliwa kwa watakao kaidi maagizo hayo.
“Kwa mujibu wa Kifungu cha 16(2)(a) cha Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha ya mwaka 2018, hatua zitakazochukuliwa kwa ukiukaji wa Sheria hiyo ni pamoja na faini isiyopungua Shilingi Milioni 20 au kifungo kwa muda usiopungua miaka miwili,” imeeleza taarifa hiyo.
Zinazohusiana:
- BOT: Marufuku kurusha hovyo noti
- BOT yashusha tena riba kwa benki za biashara Tanzania
- BoT yaaeleza sababu za kutumia jeshi kukagua maduka ya kubadilishia fedha Arusha
Huenda utekelezaji wa agizo hili ukawanusuru wananchi wengi waliokuwa wakitapeliwa na watu, taasisi za utoaji wa mikopo huku wengine wakiweka riba kubwa zinazowaumiza wananchi.
Ili kuepuka utapeli huo unaotokana na makampuni hayo yasiyo na leseni BOT imeanisha orodha ya taasisi na kampuni zenye leseni halali za biashara ya kukopesha zinazotolewa na benki hiyo.
Aidha, orodha ya taasisi, kampuni na watu binafsi wenye leseni za biashara ya kukopesha zilizotolewa na BoTinapatikana kwenye tovuti ya Benki Kuu ambayo ni www.bot.go.tz.
Latest
