Bei ya ngano kitendawili mkoani Lindi
October 11, 2024 4:19 pm ·
Fatuma Hussein
Kununua gunia la ngano la kilo 100 mkoani Lindi itakulazimu kulipa Sh400,000 ikiwa ndiyo bei ya juu zaidi kurekodiwa nchini Octoba 11,2024 ambayo ni sawa na bei iliyorekodiwa Septemba 2, mwaka huu.
Bei hiyo ni mara tano zaidi ya ile iliyotumika mkoani Rukwa ya Sh70,000 kwa gunia la kilo 100 la bidhaa hiyo muhimu katika kuandaa vitafunwa vinavyotumika katika maisha ya watu kila siku.
Wakati Lindi wakilia na ngano, wakazi wa Ruvuma na Iringa kwao ni vicheko baada ya gunia la kilo 100 la mahindi kuuzwa kwa bei ya chini ya Sh48,000 ambayo ni mara 20 zaidi ya bei ya juu iliyorekodiwa mkoani Dar es Salaam, Kilimanjaro na Pwani.

Latest
13 hours ago
·
Kelvin Makwinya
Sh385 milioni kuimarisha uchunguzi wa saratani kupitia AI, MUHAS
18 hours ago
·
Fatuma Hussein
Viwango vya kubadilisha fedha Tanzania Februari 19, 2026
2 days ago
·
Kelvin Makwinya
Sh25.8 bilioni kusambaza nishati safi ya kupikia taasisi 453 Tanzania Bara
2 days ago
·
Fatuma Hussein
Maadhimisho ya siku ya wanawake Tanzania 2026 kupambwa na vazi la batiki