Bei ya maharage yang’ang’ania kiwango cha Ijumaa

April 29, 2022 1:15 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Bei ya juu ya gunia la kilo 100 la maharage inauzwa kwa Sh280,000 katika soko la Tandale jijini Dar es Salaam.
  • Bei ya chini ya zao hilo imerekodiwa katika Mkoa wa Kagera ambako gunia la kilo 100 kwa Sh140,000.
  • Bei ya juu haijabadilika tangu Ijumaa ya  Aprili 22, 2022.

Dar es Salaam. Bei ya juu ya maharage inayotumika leo katika Mkoa wa Dar es Salaam imeendelea kubaki katika kiwango kile kile kilichorekodiwa Ijumaa ya  wiki iliyopita, jambo linaloonyesha mwenendo wa thabiti wa bei ya zao hilo. 

​Kwa mujibu wa takwimu za mazao makuu ya chakula zilizotolewa leo (Aprili 29, 2022) na Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara zinaeleza kuwa bei ya juu ya gunia la kilo 100 la maharage inauzwa kwa Sh280,000 katika soko la Tandale jijini Dar es Salaam.

Bei hiyo inayotumika leo ilitumika pia wiki iliyopita Aprili 22, 2022 katika soko hilo hilo. 

Hiyo ina maana kuwa wafanyabiashara hawajaongeza wala kupunguza faida ndani ya wiki moja huku wanunuzi nao wakiendelea kubaki katika sintofahamu kama bei itapanda au itashuka wiki ijayo.

Wakati bei ya juu ya maharage ikirekodiwa Dar es Salaam, bei ya chini ya zao hilo imerekodiwa katika Mkoa wa Kagera ambako gunia la kilo 100 linauzwa kwa Sh140,000.

Hata hivyo bei hiyo imebabadilika ambapo imepanda kutoka Sh100,000 iliyorekodiwa mkoani Kigoma.

Ifahamike kuwa utaratibu wa kutoa bei za jumla za mazao makuu ya chakula hufanyika mara tatu kwa wiki yaani Jumatatu, Jumatano na Ijumaa.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.