Bei ya maharage yang’ang’ania kiwango cha Ijumaa

April 29, 2022 1:15 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Bei ya juu ya gunia la kilo 100 la maharage inauzwa kwa Sh280,000 katika soko la Tandale jijini Dar es Salaam.
  • Bei ya chini ya zao hilo imerekodiwa katika Mkoa wa Kagera ambako gunia la kilo 100 kwa Sh140,000.
  • Bei ya juu haijabadilika tangu Ijumaa ya  Aprili 22, 2022.

Dar es Salaam. Bei ya juu ya maharage inayotumika leo katika Mkoa wa Dar es Salaam imeendelea kubaki katika kiwango kile kile kilichorekodiwa Ijumaa ya  wiki iliyopita, jambo linaloonyesha mwenendo wa thabiti wa bei ya zao hilo. 

​Kwa mujibu wa takwimu za mazao makuu ya chakula zilizotolewa leo (Aprili 29, 2022) na Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara zinaeleza kuwa bei ya juu ya gunia la kilo 100 la maharage inauzwa kwa Sh280,000 katika soko la Tandale jijini Dar es Salaam.

Bei hiyo inayotumika leo ilitumika pia wiki iliyopita Aprili 22, 2022 katika soko hilo hilo. 

Hiyo ina maana kuwa wafanyabiashara hawajaongeza wala kupunguza faida ndani ya wiki moja huku wanunuzi nao wakiendelea kubaki katika sintofahamu kama bei itapanda au itashuka wiki ijayo.

Wakati bei ya juu ya maharage ikirekodiwa Dar es Salaam, bei ya chini ya zao hilo imerekodiwa katika Mkoa wa Kagera ambako gunia la kilo 100 linauzwa kwa Sh140,000.

Hata hivyo bei hiyo imebabadilika ambapo imepanda kutoka Sh100,000 iliyorekodiwa mkoani Kigoma.

Ifahamike kuwa utaratibu wa kutoa bei za jumla za mazao makuu ya chakula hufanyika mara tatu kwa wiki yaani Jumatatu, Jumatano na Ijumaa.

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...