Bei ya maharage yaendelea kuwa kichomi Dar es Salaam 

March 4, 2026 5:46 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Bei ya maharage imeendelea kuwa tulivu nchini kutokana na kutobadilika ndani ya wiki licha ya kuendelea kwa msimu wa mvua za masika katika maeneo mbalimbali nchini. 

Kwa kawaida msimu wa mvua za masika na kipindi cha mfungo wa Ramadhan na Kwaresma kama hiki, bei za bidhaa za vyakula hupaa kutokana na kuongezeka kwa mahitaji na kupaa kwa gharama za uchukuzi kwa sababu ya athari ya mvua kwenye miundombinu. 

Uchambuzi wa bei za jumla za mazao uliofanywa na Nukta Habari umebainisha kuwa kuwa bei hizo zimeendelea kuwa thabiti katika mikoa mbalimbali, huku tofauti kubwa ikionekana kati ya bei ya juu na ya chini.

Kwa mujibu wa takwimu za mazao makuu ya biashara zilizotolewa leo Machi 4, 2026, na Wizara ya Viwanda na Biashara, bei ya jumla ya gunia la kilo 100 la maharage imeendelea kuwa Sh400,000 katika soko la Mwananyamala, jijini Dar es Salaam sawa na bei iliyorekodiwa mapema wiki hii.

Kubaki juu kwa zao hilo kwa chakula kutaendelea kuwa mzigo kwa mlaji wa mwisho, huku wafanyabiashara wakinufaika na viwango hivyo vya juu.

Hata wakati Dar es Salaam wakinunua zao hilo kwa bei ya juu, Njombe wao ndo wananunua maharage kwa bei ya jumla ya chini zaidi nchini ambapo gunia la kilo 100 linauzwa kwa Sh110,000. Bei hiyo ya Njombe ni ya chini takriban mara 4 ya ile ya Dar es Salaam na imeendelea kubaki kama ilivyokuwa mwanzoni mwa wiki.

Aidha, bei hizo hazijaonyesha mabadiliko katika mkoa wa Kigoma, ambapo zinaendelea kutumika kama zilivyokuwa Jumatatu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...

Enable Notifications OK No thanks