Bei ya maharage haishikiki Mwanza, Lindi

October 5, 2022 1:22 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Bei ya maharage kwenye mikoa hiyo yafika Sh360,000
  • Mkoa wa Iringa ndio wenye bei ndogo zaidi ya zao hilo.

Dar es Salaam. Bei ya jumla ya maharage katika mikoa ya Mwanza na Lindi imepanda na kufikia Sh360,000, jambo linalonufaisha wafanyabiashara na wakulima wanaopeleka mazao kwenye mikoa hiyo.

Bei hiyo iliyorikodiwa kwenye mikoa hiyo ni ya jumla kwa kila  gunia la kilo 100.

Takwimu za mazao makuu ya chakula zilizotolewa leo Octoba 5, 2022 na Wizara ya Viwanda na Biashara  zinaonyesha kuwa bei inayotumika katika mikoa hiyo miwili ndiyo bei ya juu kuliko maeneo mengine nchini.


Zinazohusiana:


Pia bei wanayonunua wakazi wa mikoa hiyo ni mara mbili ya inayotumika mkoani Iringa.

Wakazi wa Iringa wananunua gunia la kilo 100 la maharage kwa Sh180,000.

Maharage ni miongoni mwa mazao makuu ya chakula nchini Tanzania.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: LIVE:WABUNGE WAKIWACHAPA MASWALI MAWAZIRI | Bunge la 13 | Kikao cha 28

🔴LIVE: LIVE:WABUNGE WAKIWACHAPA MASWALI MAWAZIRI | Bunge la 13 | Kikao cha 28

Nukta TV

Top 10 ya magari yanayotumia kiwango kidogo cha mafuta

Top 10 ya magari yanayotumia kiwango kidogo cha mafuta

Nukta TV

SGR yaingizia Serikali Sh169.37 bilioni tangu kuanza kwa safari Juni 2024

SGR yaingizia Serikali Sh169.37 bilioni tangu kuanza kwa safari Juni 2024

Nukta TV