Nchi za Afrika zinazoongoza utoaji chanjo ya Uviko-19
- Orodha inaongozwa na Afrika Kusini ambayo imetoa dozi zaidi ya milioni 9 kwa raia wake.
- Nchi nyingine ni pamoja na Kenya, Ethiopia na Nigeria.
- Hadi sasa Tanzania haijafikisha watu 500,000 waliopata chanjo.
Dar es Salaam. Licha ya baadhi ya watu kuwa na mashaka juu ya chanjo ya ugonjwa wa Corona (Uviko-19), wapo waliokubali kupata chanjo hiyo ili kuepuka madhara yatokanayo na ugonjwa huo.
Waziri wa Afya Dk Gwajima mwishoni mwa mwezi Julai alisema, kupata chanjo ya Corona kutamsaidia mtu kutokufikia hatua ya kulazwa hata atakapopata ugonjwa huo.
Kwa dunia, takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonyesha kuwa takriban dozi bilioni 5 za chanjo ya Uviko-19 zimetolewa duniani na watu bilioni 1.1 duniani wamepata dozi kamili ya chanjo dhidi ya ugonjwa huo
Zipo chanjo zinazotolewa kwa dozi mbili kama Pfizer na Moderna na zinazotolewa kwa dozi moja ikiwemo Johnson & Johnson ambayo pia inatolewa nchini Tanzania.
Kwa Tanzania, WHO inaeleza kuwa dozi 218,621 za chanjo ya Corona zimetolewa ikiwa zoezi la chanjo nchini lilianza mwishoni mwa mwezi Julai.
Hata hivyo, kasi ya utoaji chanjo barani humo hairidhishi kwa sababu ni nchi nne tu katika 54 ambazo zimefanikiwa kuchanja zaidi ya asilimia 10 ya wa raia wake.
Katika video hii, utaona nchi ambazo zimetoa dozi nyingi zaidi za chanjo barani Afrika pamoja na aina ya chanjo zinazotolewa nchini humo:
Latest