Uzushi: Hakuna mabadiliko ya uwasilishaji nyaraka za vibali vya kazi Tanzania

February 2, 2021 8:35 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni uzushi unaosema kuwa kutokana na Corona utaratibu kuwasilisha nyaraka hizo umebadilika.
  • Ofisi ya Waziri Mkuu yasema hakuna mabadiliko yoyote.

Dar es Salaam. Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu imeeleza kuwa hakuna mabadiliko yoyote ya utaratibu wa uwasilishaji wa maombi ya vibali vya kazi, rufaa na msamaha ili kujikinga na janga la Corona. 

 Tamko la ofisi hiyo limekuja wakati kukiwa na taarifa za mtandaoni zinazoeleza kuwa kutokana na kuwepo kwa COVID-19, nyaraka hizo zinatakiwa ziwasilishwe makao makuu ya Idara ya Kazi zikiwa zimethibitishwa na wanasheria wa Serikali na risiti ya malipo. 

Taarifa hiyo inaeleza zaidi kuwa mabadiliko hayo yatasaidia kujikinga na maambukizi ya COVID-19 wakati uwasilishaji wa nyaraka hizo. 

Hata hivyo, taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu Februari 1, 2020 imeeleza kuwa habari hizo si za kweli na ni potofu zenye lengo la kuleta taharuki katika jamii. 

“Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu inapenda kuujulisha umma kwamba hakuna mabadiliko yaliyofanyika kwa tarehe tajwa kuhusiana na uwasilishwaji wa maombi ya vibali vya kazi, rufaa na msamaha,” anaeleza taarifa hiyo. 


Zinazohusiana:


Imesema maombi hayo yanaendelea kuwasilishwa na kushughulikiwa kwa utaratibu wa kawaida ulizoeleka wa kujaza fomu mtandaoni na kuziwasilisha kwa njia ya barua au kuzifikisha ofisini. 

“Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu inawataka watu wanaoeneza taarifa hizo za uongo kuacha upotoshaji huo mara moja. Hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao endapo watakaidi maelekezo haya,” imesisitiza taarifa hiyo.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV