Corona: Serikali ya Tanzania haijaamuru wafanyakazi, wanafunzi kukaa nyumbani

February 19, 2021 9:23 am · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Serikali haijatoa tamko lolote kuhusu wanafunzi na wafanyakazi kukaa nyumbani kipindi hiki cha Corona.
  • Habari zinazosambaa kuhusu jambo hilo ni uongo.

Dar es Salaam. Kama umeshakutana na taarifa inayosambaa kwenye mtandao wa Whatsapp juu Serikali ya Tanzania kuamuru wafanyakazi na wanafunzi kukaa nyumbani ili kujikinga na Corona, fahamu kuwa huo ni uzushi.

Serikali haijatoa tamko lolote kuhusu wanafunzi na wafanyakazi kukaa nyumbani kipindi hiki ambacho dunia inapambana na janga la COVID-19. 

Habari hiyo inayosambaa mitandaoni hasa Whatsapp kwa mfumo wa maandishi iliyoambatanishwa na kiunganishi inasema Serikali imetangaza ofisi zilizo na wafanyakazi zaidi ya 10 kuchukua likizo za lazima kuanzia Februari 17, 2021 kwa wiki mbili na shule zote kufungwa kwa muda wa wiki mbili kuanzia tarehe hiyo.

Sehemu ya habari hiyo inasema “The Tanzania Government have announced measures that all workplaces with 10 employees or more are to have paid mandatory leave to avoid the spread of the COVID-19 coronavirus starting from February 17, 2021. All schools are to close for 2 weeks also from February 17th,”

Ujumbe huo unamaanisha kuwa “Serikali ya Tanzania imetangaza njia za kujikinga na Corona kwa ofisi zilizo na wafanyakazi zaidi ya 10 kwenda likizo ya lazima kuanzia Februari 17, 2021. Shule zote kufungwa kwa wiki mbili kwanzia Februari 17.”

Hata hivyo, habari hiyo haina ukweli wowote kwasababu Serikali haikutoa tamko lolote kama hilo siku za hivi karibuni.


Zinazohusiana:


Pia kiunganishi cha habari hiyo ambacho kinamuelekeza mtu kwenda kwenye tovuti nyingine ili kusoma zaidi, lakini hakuna habari kama hiyo. Kiunganishi hicho kina maudhui ambayo hayafai kuonyeshwa kwa umma. 

Watumiaji wa mitandao ya kijamii wanapaswa kutumia taarifa sahihi kutoka vyanzo sahihi vya Serikali ikiwemo Wizara ya Afya na Shirika la Afya Duniani (WHO) ili kujikinga na COVID-19.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV