Famba:Tamisemi haijawapangia walimu vituo vipya vya kazi

January 4, 2023 12:40 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Mpaka sasa hakuna watumishi waliopangiwa vituo vya kazi kwa mwaka 2023
  • Tamisemi yataka taarifa za uzushi zipuuzwe.

Dar es Salaam.Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) imewataka wananchi kupuuzia taarifa inayoenea mtandaoni inayohusu kuwapangia walimu  vituo vya kazi kwa mwaka wa ajira 2023/24.

Taarifa hiyo ya uzushi inayosambazwa kupitia barua inayofanana na   barua rasmi zinazotolewa na Tamisemi  inaeleza kuwa Serikali imewapangaia vituo vya kazi walimu ambao hawakupangiwa kwa mwaka 2022 jambo ambalo siyo la kweli.


Kwa mujibu wa  tovuti rasmi ya Tamisemi hakuna wafanyakazi wa kada yoyote waliopangiwa vituo vya kazi kwa mwaka 2023/24.

Mara ya mwisho kwa Wizara hiyo kutoa orodha ya majina ya watumishi wa umma waliopangiwa vituo vya kazi kwenye kada za ualimu ilikuwa  Juni 26, 2022.

Hata wakati Tamisemi wakikanusha uzushi huo Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye ulemavu  kupitia tovuti yao haijatoa orodha yoyote ya majina ya walimu waliopangiwa vituo vya kazi,  jambo linalothibitisha huenda taarifa hiyo ikawa ni ya upotoshaji. 

Hii si mara kwanza kwa taarifa za uzushi kuhusu wizara hiyo kutengenezwa, ikiwa na lengo la kupotosha na kuzua taharuki kwa watumishi wa umma kwenye kada za ualimu pamoja na afya ambao hawakupangiwa ajira.


Soma zaidi


Tulichobaini

Huenda taarifa hiyo ya uzushi ikawa imetengenezwa na watu wenye nia ya upotoshaji au kuwatapeli watu wasio na ajira.

Aina ya mwandiko iliyotumika kwenye barua  hiyo haifanani kabisa na mwandiko halisi unaotumika kwenye barua  rasmi za Tamisemi.

Makosa ya kisarufi yaliyopo kwenye barua hiyo ni ushahidi tosha kuwa huenda barua hiyo imeandikwa na mtu mwenye taaluma ndogo au asiyefahamu itifaki za mawasiliano.

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...