Famba:Tamisemi haijawapangia walimu vituo vipya vya kazi
- Mpaka sasa hakuna watumishi waliopangiwa vituo vya kazi kwa mwaka 2023
- Tamisemi yataka taarifa za uzushi zipuuzwe.
Dar es Salaam.Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) imewataka wananchi kupuuzia taarifa inayoenea mtandaoni inayohusu kuwapangia walimu vituo vya kazi kwa mwaka wa ajira 2023/24.
Taarifa hiyo ya uzushi inayosambazwa kupitia barua inayofanana na barua rasmi zinazotolewa na Tamisemi inaeleza kuwa Serikali imewapangaia vituo vya kazi walimu ambao hawakupangiwa kwa mwaka 2022 jambo ambalo siyo la kweli.
— OFISI YA RAIS TAMISEMI (@ortamisemitz) January 4, 2023
Kwa mujibu wa tovuti rasmi ya Tamisemi hakuna wafanyakazi wa kada yoyote waliopangiwa vituo vya kazi kwa mwaka 2023/24.
Mara ya mwisho kwa Wizara hiyo kutoa orodha ya majina ya watumishi wa umma waliopangiwa vituo vya kazi kwenye kada za ualimu ilikuwa Juni 26, 2022.
Hata wakati Tamisemi wakikanusha uzushi huo Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye ulemavu kupitia tovuti yao haijatoa orodha yoyote ya majina ya walimu waliopangiwa vituo vya kazi, jambo linalothibitisha huenda taarifa hiyo ikawa ni ya upotoshaji.
Hii si mara kwanza kwa taarifa za uzushi kuhusu wizara hiyo kutengenezwa, ikiwa na lengo la kupotosha na kuzua taharuki kwa watumishi wa umma kwenye kada za ualimu pamoja na afya ambao hawakupangiwa ajira.
Soma zaidi
Tulichobaini
Huenda taarifa hiyo ya uzushi ikawa imetengenezwa na watu wenye nia ya upotoshaji au kuwatapeli watu wasio na ajira.
Aina ya mwandiko iliyotumika kwenye barua hiyo haifanani kabisa na mwandiko halisi unaotumika kwenye barua rasmi za Tamisemi.
Makosa ya kisarufi yaliyopo kwenye barua hiyo ni ushahidi tosha kuwa huenda barua hiyo imeandikwa na mtu mwenye taaluma ndogo au asiyefahamu itifaki za mawasiliano.
Latest
