Famba:Tamisemi haijawapangia walimu vituo vipya vya kazi

January 4, 2023 12:40 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Mpaka sasa hakuna watumishi waliopangiwa vituo vya kazi kwa mwaka 2023
  • Tamisemi yataka taarifa za uzushi zipuuzwe.

Dar es Salaam.Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) imewataka wananchi kupuuzia taarifa inayoenea mtandaoni inayohusu kuwapangia walimu  vituo vya kazi kwa mwaka wa ajira 2023/24.

Taarifa hiyo ya uzushi inayosambazwa kupitia barua inayofanana na   barua rasmi zinazotolewa na Tamisemi  inaeleza kuwa Serikali imewapangaia vituo vya kazi walimu ambao hawakupangiwa kwa mwaka 2022 jambo ambalo siyo la kweli.


Kwa mujibu wa  tovuti rasmi ya Tamisemi hakuna wafanyakazi wa kada yoyote waliopangiwa vituo vya kazi kwa mwaka 2023/24.

Mara ya mwisho kwa Wizara hiyo kutoa orodha ya majina ya watumishi wa umma waliopangiwa vituo vya kazi kwenye kada za ualimu ilikuwa  Juni 26, 2022.

Hata wakati Tamisemi wakikanusha uzushi huo Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye ulemavu  kupitia tovuti yao haijatoa orodha yoyote ya majina ya walimu waliopangiwa vituo vya kazi,  jambo linalothibitisha huenda taarifa hiyo ikawa ni ya upotoshaji. 

Hii si mara kwanza kwa taarifa za uzushi kuhusu wizara hiyo kutengenezwa, ikiwa na lengo la kupotosha na kuzua taharuki kwa watumishi wa umma kwenye kada za ualimu pamoja na afya ambao hawakupangiwa ajira.


Soma zaidi


Tulichobaini

Huenda taarifa hiyo ya uzushi ikawa imetengenezwa na watu wenye nia ya upotoshaji au kuwatapeli watu wasio na ajira.

Aina ya mwandiko iliyotumika kwenye barua  hiyo haifanani kabisa na mwandiko halisi unaotumika kwenye barua  rasmi za Tamisemi.

Makosa ya kisarufi yaliyopo kwenye barua hiyo ni ushahidi tosha kuwa huenda barua hiyo imeandikwa na mtu mwenye taaluma ndogo au asiyefahamu itifaki za mawasiliano.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.