Rais Samia aungana na Watanzania kumuaga Dk Ndugulile
Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan ameungana na viongozi wa Serikali, familia, na wananchi katika kutoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Mbuge wa jimbo la Kivukoni na Mkurugenzi Mteule wa Shirika la Afya kanda ya Afrika, aliyeaga dunia Novemba 27, 2024.
Shughuli ya kumuaga Dk Ndugulile inafanyika leo katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Dk Ndugulile alifariki dunia Novemba 27, 2024 nchini India alipokuwa akipatiwa matibabu ikiwa ni miezi mitatu tangu achaguliwe kuwa Mkurugenzi Mteule wa WHO kanda ya Afrika.