Matokeo kidato cha nne mwaka 2020 haya hapa

January 15, 2021 2:50 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Ufaulu waongezeka kwa asilimia 5.19.
  • Watahiniwa wa shule 373,958 wamefaulu mtihani kati ya wanafunzi 434,654 waliofanya mtihani huo.

Dar es Salaam. Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya kidato cha nne mwaka 2020 huku ufaulu ukiongezeka kwa asilimia 5.19 kutoka ule wa mwaka 2019.

Necta imeeleza leo kuwa katika mtihani huo watahiniwa wa shule 373,958 wamefaulu mtihani kati ya wanafunzi 434,654 waliofanya mtihani huo Novemba mwaka jana ikiwa ni sawa na asilimia 85.84 ya watahiniwa wote. 

Hii ni sawa na kusema kuwa takriban wanafunzi 85 kati ya 100 waliofanya mtihani huo wamefaulu. 

Ufaulu huo, kwa mujibu wa Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde, ni sawa ongezeko la asilimia 5.19 ikilinganishwa na matokeo ya mwaka 2019. Mwaka juzi asilimia 80.65 ya watahiniwa wa shule walifaulu mtihani huo.


Soma zaidi:


Hata hivyo, ni wanafunzi 152,903 sawa na asilimia 35.1 ya watahiniwa wote waliofanya mtihani huo wamefanikiwa kupata daraja la I hadi la III.

Kati ya wanafunzi hao waliopata ufaulu mzuri zaidi, wasichana ni 66,899.  

Kupata matokeo ingia hapa >>>>> https://bit.ly/2XIyOu0

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV