Mataifa 10 yaliyoongoza kuleta watalii wengi Tanzania Oktoba 2022
December 7, 2022 5:16 am ·
Mwandishi
- Ni pamoja na Kenya, Ufaransa, Marekani na Burundi.
- Idadi ya watalii walioingia nchini Oktoba 2022 ilikuwa 141,517.
Dar es Salaam. Kwa mujibu wa takwimu za Ofisi ya Taifa ya Takwimu za Oktoba 2022 (High Frequency Data), idadi ya watalii walioingia nchini Oktoba ilikuwa 141,517 ikiongezeka kutoka 133,998 iliyorekodiwa Septemba.
Hilo ni sawa na ongezeko la watalii 7,519 au asilimia 5.6.
Kuongezeka kwa idadi hiyo kumekuja baada ya idadi ya watalii kushuka miezi miwili mfululizo. Julai mwaka huu Tanzania ilirekodi watalii 166,736 na mwezi uliofuata wakapungua hadi 158,049 kabla hawajapungua zaidi hadi 133,998 mwezi Septemba.
NBS imeeleza kuwa Oktoba mwaka huu, Kenya ndiyo iliongoza kuingiza watalii wengi zaidi nchini ikifuatiwa na Ufaransa, Marekani na Burundi.
Latest

3 days ago
·
Esau Ng'umbi
CCM yaahidi kutengeneza ajira milioni 8 ifikapo 2030

4 days ago
·
Kelvin Makwinya
Bajeti ya Wizara ya Ardhi yapungua kwa Sh7.2 bilioni 2025/26

6 days ago
·
Fatuma Hussein
Bajeti Wizara ya Maendeleo yaongezeka kwa asilimia 11.9

6 days ago
·
Kelvin Makwinya
Tanzania kujenga kituo cha upandikizaji figo kikubwa zaidi Afrika