Idadi ya watalii Tanzania yaongezeka kwa asilimia 25.7

October 11, 2023 8:33 am · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ongezeko hilo linafanya kuwa na jumla ya watalii 1,131,286 waliotembelea Tanzania.
  • Asilimia 3.3 kati yao waliingia nchini kupitia visiwani Zanzibar.

Dar es Salaam.Idadi ya watalii walioingia Tanzania imeongezeka kwa asilimia 25.7 ndani ya kipindi cha mwaka mmoja huku nchi za Amerika na Ufaransa zikiingiza idadi kubwa zaidi ya watalii.

Kwa mujibu wa takwimu zinazotolewa na za Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) hadi kufikia Agosti 2023 watalii 1,131,286  waliingia nchini ulinganisha na watalii 900,182  waliorekodiwa Agosti mwaka jana.

NBS inafafanua kuwa asilimia 3.3 ya watalii hao waliingia nchini kupitia visiwani Zanzibar kunakosifika kwa vivutio mbalimbali vya utalii ikiwemo misitu ya viungo vya kupikia na  maeneo ya kihistoria.

“Kati ya watali wote walioingia nchini, watalii 336,203 waliingia kupitia Zanzibar, sawa na asilimia 31.1 ya watalii wote,” imesema taarifa ya NBS.

Miongoni mwa mataifa yalioongoza kwa kuingiza watalii wengi kutoka nje ya bara la Afrika ni pamoja na Marekani  watalii 84,541, Ufaransa (72,009), Ujerumani (57,798), Uingereza (51,505) na Italia  watalii 51,056.

Watalii kutoka ndani ya bara la Afrika ni pamoja na Kenya watalii 128,753, Burundi (69,505), Zambia (38,394), Rwanda (37,269) na Uganda watalii 28,594

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
9 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
9 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
EXCLUSIVE: Fahamu ukweli kuhusu kunyonyesha na kumbemenda mtoto | PART 1

EXCLUSIVE: Fahamu ukweli kuhusu kunyonyesha na kumbemenda mtoto | PART 1

Nukta TV

Rais Samia aipa miezi 5 Tume ya Uchunguzi jinai Oktoba 29

Rais Samia aipa miezi 5 Tume ya Uchunguzi jinai Oktoba 29

Nukta TV

Rais Samia ataja sababu kushirikisha wajumbe kutoka nje, Tume ya Uchunguzi makosa ya jinai Oktoba 29

Rais Samia ataja sababu kushirikisha wajumbe kutoka nje, Tume ya Uchunguzi makosa ya jinai Oktoba 29

Nukta TV