Idadi ya watalii wa kigeni yapaa Tanzania

March 6, 2025 4:12 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link

Tanzania imeendelea kung’ara katika sekta ya utalii baada ya kurekodi ongezeko kubwa la idadi ya watalii wa kigeni mwaka 2024. Kwa mujibu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), jumla ya watalii 2,141,895 waliingia nchini, ikiwa ni ongezeko la asilimia 18.58 ikilinganishwa na mwaka 2023.

Hii ni mara tatu zaidi ya idadi ya watalii walioingia nchini mwaka 2020 wakati dunia ilipokumbwa na janga la Uviko-19, ambapo ni 620,867 pekee waliotembelea Tanzania.

Kwa upande wa miezi, Julai umeibuka kinara kwa kuvutia wageni wengi zaidi, huku watalii 218,065 wakiwasili nchini. Kinyume chake, Aprili ndiyo ilikuwa na idadi ndogo zaidi, ikiwa na watalii 116,280 pekee.

Ongezeko hili linaonyesha mvuto wa Tanzania kama kivutio cha utalii duniani, huku vivutio kama Hifadhi ya Serengeti, Mlima Kilimanjaro, na fukwe za Zanzibar vikichangia kwa kiasi kikubwa.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
WAMESANUKA, mbinu mpya ya usafirishaji wa dawa za kulevya yafichuliwa

WAMESANUKA, mbinu mpya ya usafirishaji wa dawa za kulevya yafichuliwa

Nukta TV

CCM yatoa ratiba maombi ya kumrithi Lukuvi, Israel, Lebanon wakisitisha mapigano

CCM yatoa ratiba maombi ya kumrithi Lukuvi, Israel, Lebanon wakisitisha mapigano

Nukta TV

Ridhiwani: Serikali inalenga kuacha tabasamu kwa watumishi wa Umma

Ridhiwani: Serikali inalenga kuacha tabasamu kwa watumishi wa Umma

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.