Watalii waongezeka Tanzania, mapato yavunja rekodi mwaka 2025

July 17, 2026 5:31 pm · Method Allen
Share
Tweet
Copy Link

  • Idadi ya watalii wa kimataifa imeongezeka kwa asilimia 6.7

Dar es Salaam.Tanzania imeendelea kuvutia wageni kutoka nchi mbalimbali duniani, huku sekta ya utalii ikirekodi mafanikio makubwa mwaka 2025.

Kwa mujibu wa ripoti ya Utafiti wa Watalii wa Kimataifa Wanaoondoka Nchini, iliyotolewa na Benki kuu ya Tanzania (BoT) na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Idadi ya watalii wa kimataifa imeongezeka kwa asilimia 6.7.

Mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka 2025 jumla ya watalii milioni 2.29 waliitembelea Tanzania kutoka milioni 2.14 iliyorekodiwa mwaka 2024.

Watalii hao waliingizia Tanzania Dola za Marekani bilioni 4.41 sawa na Sh11.6 trilioni   ndani ya mwaka mmoja.

Ripoti ya NBS na BoT inabainisha kuwa wageni wengi wakitembelea nchini kwaajili ya mapumziko na likizo, wakivutiwa na uzuri wa tanzania na maeneo ya kujiachia yakiwa kama Serengeti, Ngorongoro, Tarangire, Mji mkongwe wa Zanzibari na fukwe za Bahari ya Hindi. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
2 Sep, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
2 Sep, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Majibu ya Serikali: Uhaba wa wataalamu wa ganzi, ajira 10,009 kutolewa

Majibu ya Serikali: Uhaba wa wataalamu wa ganzi, ajira 10,009 kutolewa

Nukta TV

Shangazi aibana Serikali kuhusu hadhi ya madereva, Prof. Kitila aingilia kati

Shangazi aibana Serikali kuhusu hadhi ya madereva, Prof. Kitila aingilia kati

Nukta TV

Haya ndio mambo ya kufanya bosi wako akikutongoza

Haya ndio mambo ya kufanya bosi wako akikutongoza

Nukta TV