Huu ndiyo mwelekeo wa Serikali ya awamu ya sita Tanzania

April 22, 2021 2:18 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni kudumisha mambo yaliyofanywa katika awamu zilizopita, kuyaendeleza mema yaliyopo na kuleta mengine mapya.
  • Baadhi ya mambo yatabadilishwa ili kuongeza ufanisi wa Serikali.

Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan amesema dira na muelekeo wa Serikali ya awamu ya sita anayoingoza ni kudumisha mambo yaliyofanywa katika awamu zilizopita, kuyaendeleza mema yaliyopo na kuleta mengine mapya.

Rais Samia aliyekuwa akizungumza leo Aprili 22, 2021 jijini Dodoma wakati akilihutubia Bunge kwa mara ya kwanza tangu alipoapishwa kuwa Rais Machi 19 mwaka huu amesema yapo baadhi ya mambo yatabadilishwa ili kuongeza ufanisi wa Serikali.

“Dira na muelekeo wa Serikali  ya awamu ya sita ni kudumisha mazuri ya awamu zilizopita, kuendeleza mema yaliyopo na kuleta mengine mapya. Hii ndio dhana na maana halisi ya kauli mbiu au salamu yetu ya “Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kazi iendelee,” amesema Rais Samia mbele ya Wabunge wa Bunge la Tanzania. 

Amesema mipango mbalimbali inayotekelezwa na awamu ya sita ni ile iliyokuwepo awamu ya tano iliyokuwa ikiongozwa na Hayati Rais John Magufuli aliyefariki dunia Machi 17 mwaka huu. 


Soma zaidi:


Amesema mipango hiyo itaongozwa na Dira ya Maendeleo ya 2025, Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020/25, mpango wa 3 wa maendeleo wa miaka mitano, agenda ya maendeleo ya Afrika ya 2063 na agenda ya dunia ya malengo endelevu ya 2030.  

“Kwa kuwa nilivyowahi kusema huko nyuma, nirudie tena kuwa mimi na Hayati Dk Rais John Magufuli tulikuwa kitu kimoja. Kwa maana hiyo mambo mengi ambayo Serikali imepanga kuyatekeleza ni yale ambayo yalielezwa na Rais Hayati John Magufuli wakati akilizundua bunge hili,” amesema Rais Samia. 

Amesema Serikali inayoingoza itaelekeza nguvu kubwa katika kusimamia ukuaji wa uchumi, kudumisha amani na utulivu na kuimarisha miundombinu mbalimbali ikiwemo ya barabara ili kuwezesha shughuli za biashara na utoaji huduma za kijamii.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV