Watalii waongezeka Tanzania, mapato yavunja rekodi mwaka 2025
- Idadi ya watalii wa kimataifa imeongezeka kwa asilimia 6.7
Dar es Salaam.Tanzania imeendelea kuvutia wageni kutoka nchi mbalimbali duniani, huku sekta ya utalii ikirekodi mafanikio makubwa mwaka 2025.
Kwa mujibu wa ripoti ya Utafiti wa Watalii wa Kimataifa Wanaoondoka Nchini, iliyotolewa na Benki kuu ya Tanzania (BoT) na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Idadi ya watalii wa kimataifa imeongezeka kwa asilimia 6.7.
Mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka 2025 jumla ya watalii milioni 2.29 waliitembelea Tanzania kutoka milioni 2.14 iliyorekodiwa mwaka 2024.
Watalii hao waliingizia Tanzania Dola za Marekani bilioni 4.41 sawa na Sh11.6 trilioni ndani ya mwaka mmoja.
Ripoti ya NBS na BoT inabainisha kuwa wageni wengi wakitembelea nchini kwaajili ya mapumziko na likizo, wakivutiwa na uzuri wa tanzania na maeneo ya kujiachia yakiwa kama Serengeti, Ngorongoro, Tarangire, Mji mkongwe wa Zanzibari na fukwe za Bahari ya Hindi.
