NECTA yapiga marufuku kuchapisha matokeo kwa majina ya wanafunzi bila idhini

September 4, 2025 7:14 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni kwa lengo la kulinda faragha na taarifa binafsi za kielimu za wahitimu na watahiniwa wote waliowahi kufanya mitihani.

Dar es Salaam. Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta) limepiga marufuku vyombo vya habari, mitandao ya kijamii, blogu na majukwaa ya habari kuchapisha au kusambaza matokeo ya mitihani kwa kutumia majina ya wanafunzi bila idhini yao, likieleza kuwa kitendo hicho ni kosa la jinai.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Afisa Habari na Uhusiano wa Necta, John Nchimbi, hatua hiyo imechukuliwa ili kulinda faragha na taarifa binafsi za kielimu za wahitimu na watahiniwa wote waliowahi kufanya mitihani yake, kwa mujibu wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, Sura ya 44 ya mwaka 2023.

“Baraza la Mitihani linatambua umuhimu wa kuwapa wananchi taarifa sahihi kuhusu maendeleo ya kielimu ya wanafunzi na watahiniwa kwa kuzingatia misingi ya sheria, maadili na heshima kwa kulinda faragha zao,” imeeleza taarifa hiyo.

Aidha, Necta imeeleza kuwa inaendela kuboresha mifumo yake ya Tehama kwa kuondoa utaratibu wa kuonesha majina ya wanafunzi au watahiniwa katika tovuti yake rasmi ya www.necta.go.tz, ili kuhakikisha usalama wa taarifa binafsi.

Hata hivyo, agizo la Necta limekuja mara baada ya hivi karibuni vyombo vya habari na watu binafsi kuchapisha wasifu wa watu mbalimbali ikiwemo viongozi. Uchapishaji huo wa wasifu ulizua mijadala katika majukwaa ya mitandao ya kijamii huku kila mmoja akitoa mtazamo tofauti kulingana na wasifu wa elimu wa mtu husika. 

Necta imesisitiza kuwa ni kosa la jinai kwa mtu yeyote au taasisi kuhifadhi, kuchapisha, kusambaza au kuonesha hadharani matokeo ya mtahiniwa kwa kutumia jina lake au taarifa nyingine zinazoweza kumtambua bila idhini yake na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya yeyote atakayekiuka agizo hilo.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
26 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
26 May, 2026
No active movers today
Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MIKOA 5 YA KIPOLISI INAYOONGOZA KWA MAKOSA BARABARANI

MIKOA 5 YA KIPOLISI INAYOONGOZA KWA MAKOSA BARABARANI

Nukta TV

SERIKALI YAKAMILISHA MAZUNGUMZO MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

SERIKALI YAKAMILISHA MAZUNGUMZO MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

Nukta TV

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

Nukta TV