Fursa kwa wakulima, uhitaji mazao ya chakula ukiongezeka Kenya, Uganda

July 28, 2026 2:07 pm · Method Allen
Share
Tweet
Copy Link

Huenda Tanzania ikawa na nafasi kubwa ya kuongeza mauzo ya mazao ya chakula katika nchi za Kenya na Uganda baada ya mauzo katika soko hilo kushuka kwa asilimia 70.

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) inabainisha kuwa katika mataifa hayo bado kuna uhitaji mkubwa wa chakula husasan mahindi, mchele, dengu na maharage ya soya.

Takwimu za TanTrade zinaonyesha mauzo ya mazao hayo katika soko la Uganda yalipungua kwa asilimia 71 ndani ya miaka mitano kutoka Dola za Marekani milioni 154 kwa mwaka 2021 hadi  Dola za Marekani milioni 45 mwaka 2025.

Kwa upande wa soko la Kenya, mauzo yalishuka kwa asilimia 92 katika kipindi sawa na hicho yakipungua kutoka Dola za Marekani milioni 121 mwaka 2021 hadi Dola za Marekani milioni 10.

Licha ya mabadiliko ya kiwango cha mauzo katika miaka ya hivi karibuni, ripoti inaonyesha kuanzia mwaka 2026 hadi 2030, soko la Uganda linakadiriwa kuongeza mauzo ya Dola za Marekani milioni 135, huku soko la Kenya kuongeza Dola za Marekani milioni 82.

Hii inamaanisha fursa kwa wakulima wa Tanzania hususan wanaolima mazao ya mahindi, mchele, dengu na maharage ya soya, kuongeza uzalishaji na thamani ya mazao zaidi ili kupanua wigo wa kujipatia kipato kutoka katika soko hilo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
24 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
24 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Nukta TV

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Nukta TV

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Nukta TV