Jinsi ya kufungua programu zilizofichwa kwenye iPhone

January 6, 2025 12:30 pm · Davis Matambo
Share
Tweet
Copy Link
  • Zinaweza kufichwa, kufunguliwa na kurejeshwa kwa uthibitisho wa kibayometriki au nenosiri.

Dar es Salaam. Watumiaji wa simu za iPhone kutoka kampuni ya Apple yenye makao yake makuu California, Marekani, wameanza kufurahia uwezo wa kipengele kipya cha kuficha na kufunga programu kwenye simu zao kupitia toleo jipya la iOS 18 lililotolewa Septemba 2024.

Kipengele hicho husaidia kulinda programu na taarifa nyeti kutokuonekana na wengine wanapotumia simu kwa kuzificha programu kwenye folda maalumu ambalo uhitaji nenosiri au uthibitisho wa kibayometriki.

Ili kufunga au kuficha programu kwenye iPhone, bonyeza na ushikilie ikoni ya programu, kisha chagua ‘Require Face ID.’ Programu hiyo itatoweka kutoka kwenye skrini iliyozoeleka na haitapatikana hata kwenye matokeo ya utafutaji wa ‘Spotlight’. 

Programu zilizofichwa huondolewa kwenye skrini kuu na kuhifadhiwa kwenye folda ya siri inayoitwa inayopatikana kwenye ‘App Library’. Picha |CNET

Lakini, wakati mwingine programu zinaweza kufichwa kwa makusudi au kwa bahati mbaya, na zikahitajika kutumiwa tena. Kujua hatua za kuziona kupitia mipangilio ni muhimu ili kusaidia kuzifungua bila kuhangaika.

Kuna njia mbili za kupata programu zilizofichwa kwenye iPhone, ya kwanza ni kufungua iPhone yako na kushuka hadi mwisho wa skrini ili kufikia ukurasa wa ‘App Library.’

Chini kabisa bonyeza ‘hidden folder’, kisha utaombwa kuthibitisha kwa kutumia ‘Face ID’ au ‘Touch ID’, ikiwa uthibitisho wa kibiometriki utashindikana, ingiza nenosiri.

Ukishafanya hivyo, utaweza kuona programu zote zilizofichwa. Ili kuzifungua, utahitaji kuthibitisha tena kwa njia hiyo hiyo yaani kwa kutumia Face ID, Touch ID, au nenosiri ili programu hizo zisifunguliwe na mtu mwingine yeyote bila kibali cha mwenye simu.

Njia ya pili ya kuna programu zilizofichwa ni kupitia mipangilio ‘settings’, hapa nenda kwenye ‘Settings’ kisha ‘Apps’ alafu uingie kwenye ‘Hidden Apps’, kuona programu zote zilizofichwa.

‘Screenshot’ ikionyesha unavyoweza kufunga programu za msingi kama ‘Notes’ kwa kuchagua ‘Require Face ID’ kwa usalama wa nyaraka zako. Picha |CNET

Wakati mwingine mtumiaji anaweza kuficha programu bila kukusudia na kuhitaji kuirejesha kwenye utaratibu wa upatikanaji wa kawaida kwenye ‘home screen’, ili kuirejesha fuata njia ifuatayo.

Fungua iPhone yako na nenda kwenye ‘App library’, kisha gusa ili kufungua folda ya programu zilizofichwa kwa kutumia Face ID au Touch ID.

Baada ya hapo, gusa na ushikilie programu mahususi unayotaka kuirejesha, alafu chagua ‘Don’t require Face ID,’ na uthibitishe kwa mara ya mwisho kwa kutumia uso, alama ya kidole au nenosiri.

Hatua hizo zitakapo fuatwa, programu lengwa itaondolewa kwenye folda la siri na kurudi tena kwenye skrini ya mwanzo, ambapo mtumiaji anaweza kufanya hivyo kwa kuitafuta kwenye ‘App library’ au kupitia ‘Spotlight’.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
17 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
17 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
17 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Siku ya Familia, Mtoto wa Afrika kuadhimishwa Juni 30, 2026

Siku ya Familia, Mtoto wa Afrika kuadhimishwa Juni 30, 2026

Nukta TV

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Nukta TV

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Nukta TV