Apple yasogeza mbele uzinduzi wa toleo jipya iPad

August 4, 2022 1:42 pm · Davis Matambo
Share
Tweet
Copy Link
  • Itazindua Oktoba badala ya Septemba.
  • Lengo ni kupata muda wa kuboresha zaidi mfumo huo.

Watumiaji wa bidhaa za Apple ya Marekani watalazimika kusubiri hadi Oktoba mwaka huu wakati kampuni hiyo ikiboresha toleo jipya la tableti zake.

Awali Apple inayotengeneza simu aina ya iPhone ilipanga kufanya uzinduzi huo Sepetemba 2022 lakini imesema bado haijakamilisha taratibu za kuuboresha mfumo wa endeshi (IPadOS) katika tableti hizo.

Imesema inahitaji muda wa kutosha kufanya maboresho yatakoyoziwezesha tableti mpya kuwa na ufanisi wa kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja.

Kwa mujibu wa chombo cha habari cha Bloomberg, Apple inafanyia kazi kipengele kipya cha “stage manager” kilichopo kwenye tableti hizo.


Zinazohusiana;


Kipengele hicho kitaruhusu watumiaji kuvinjari kwa urahisi na haraka wakati wanatumia kifaa hicho cha mawasiliano.

Kawaida kampuni hiyo hutoa mifumo mipya ya uendeshaji wa iPhone na iPad kwa wakati mmoja Septemba kila mwaka.

Hii ina maana kuwa iPadOS 16 haitatoka hadi Oktoba, mwezi mmoja baada ya kutolewa kwa mfumo mpya endeshi  wa iPhone.

Inajumuisha ‘sasisho kubwa zaidi kuwahi kutokea’ kwa skrini iliyofungwa, ambayo hurahisisha kubadilisha picha za mandharinyuma na rangi na muundo wa fonti za onyesho.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
27 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
27 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
27 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Dk Nchimbi afukuzwa CCM, Ndejembi akipendekezwa kuchukua mikoba

Dk Nchimbi afukuzwa CCM, Ndejembi akipendekezwa kuchukua mikoba

Nukta TV

Haya hapa mafao ya Dk Emmanuel Nchimbi aking’atuka madarakani

Haya hapa mafao ya Dk Emmanuel Nchimbi aking’atuka madarakani

Nukta TV

SIMULIZI: Namna Magufuli, Samia walivyoichonga historia ya Bwawa la Mwalimu Nyerere

SIMULIZI: Namna Magufuli, Samia walivyoichonga historia ya Bwawa la Mwalimu Nyerere

Nukta TV