Twitter yafungua fursa ya kukuza “brand” za wafanyabiashara
- Iko mbioni kuanzisha jukwaa litakalowakutanisha wadau wa biashara na matangazo.
- Litatumika kushauriana na kutafuta njia bora za kukuza brand za biashara
- Twitter bado hawajatoa tamko rasmi ni lini litaanza kufanya kazi.
Kama wewe ni mfabiashara na umekuwa ukitumia mtandao wa Twitter kutangaza bidhaa na huduma, basi una kila sababu ya kutabasamu, kwa sababu mtandao huo unakupeleka katika hatua ya mafanikio zaidi.
Mtandao huo uko mbioni kuanzisha jukwaa jipya la “Twitter Next” ambalo linawakutanisha wadau na wabia wa biashara duniani kujadili na kushauriana njia bora za kukuza biashara na “brand” zao.
Kwa mujibu wa mtandao wa Social Media Today, Twitter inaungana na watengeneza maudhui na warusha matangazo ili kutafuta namna bora ya kufaidika na jukwaa hilo ambalo ni maalum kwa watu wenye nia kukuza “brand” zao.
Zinazohusiana:
- Facebook yafanya maboresho utafutaji wa bidhaa mtandaoni
- Wafanyabiashara wanavyoweza kunufaika na kalenda ya Twitter
- Twitter kuwawekea watumiaji wake muonekano mpya
Huenda huduma hiyo mpya ya Twitter itawasaidia wafanyabiashara kufanya shughuli zao kwa teknolojia ya kisasa na yenye uwezo mkubwa wa kupata uchaguzi mpana wa jinsi ya kuwafikia wateja ambao ni muhimu katika kuwaingizia kipato.
Hata hivyo, Twitter hawajatoa tamko rasmi la jukwaa hilo na lini litaanza kufanya kazi kwa watumiaji wake.