Mbinu zitakazokuepusha na Corona ukiwa kwenye gari

April 16, 2020 10:54 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Tumia vitakasa vilivyoidhinishwa kimataifa.
  • Pendelea kuosha gari yako mwenyewe na hakikisha hautumii maji mengi.
  • Hakikisha haukosi vitu muhimu vikiwemo vitakasa mikono na barakoa kwenye gari yako.

Dar es Salaam. Huenda unajihisi upo salama kwa kuwa hautumii usafiri wa umma lakini vipi kuhusu gari lako? Bado unatakiwa kuchukua tahadhari.

Wakati huu ambao huwezi kumbaini mgonjwa wa virusi hivyo kwa kumtazama, haya ni mambo ambayo unaweza kuzingatia ili kuwa salama na kujikinga na maambukizi ya virusi hivyo wakati ukitumia gari lako:

1. Tumia vitakasa vyenye kemikali ya “Hydrogen peroxide” ambayo haitadhuru baadhi ya sehemu za gari lako. Unaweza kuipata kwenye duka la dawa na kisha kuiweka kwenye chombo cha kupulizia. 

Kusafisha unaweza kupulizia kemikali hiyo sehemu mbalimbali za gari na kisha kufuta na kitambaa kisafi. 

Hakikisha unakifua kitambaa hicho kwa sabuni baada ya kutumia na unashauliwa kutumia vikinga mikono (gloves) wakati unafanya shughuli hizo.

2. Pendelea kuosha gari lako mwenyewe wakati huu wa mlipuko wa Corona. Hii itakusaidia gari yako kutokugusa hasa ndani na watu ambao huwafahamu.

Pendelea kuosha gari lako kwani huwezi kujua kama anayekufanyia kazi hiyo yupo salama.  Picha| Giphy.

Ni muhimu kuchukua tahadhari zote kipindi hiki ili kulifanya gari lako kuwa mahali salama na kuepuka maambukizi.

3. Hakikisha hukosi vifaa vya kujikinga vikiwemo barakoa na vitakasa vya kujisafisha mwenyewe na kushafisha gari lako. 

Unaweza kununua barakoa na kuvaa baada ya kushuka kwenye gari lako na kuelekea mahala penye watu wengi kama sokoni na maeneo mengine.

Pia unaweza kuhakikisha unakuwa na visafishio vya vioo vya gari vyenye vitakasa (wipes) zilizoidhinishwa kwa kiwango cha kimataifa kwani siyo kila kitakasa kinaweza kukukinga na virusi vya Corona.


Zinazohusiana


4. Ni vizuri kutumia dhana hizo kwa kiasi kwani endapo utatumia kwa zaidi, huenda unyevu akaobaki ukakuletea harufu isiyopendeza kwenye gari lako na hata kusababisha fangasi kuzaliana. Tumia kiasi tu.

Kama unafahamu njia nyingine ya kuwasaidia wadau wanaotumia usafiri binafsi, usiache kuacha maoni yako kwenye kurasa zetu za mitandao ya  kijamii.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV