Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo yapewa asilimia 45 ya bajeti 2022-23

June 6, 2023 1:45 pm · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Yapata asilimia 32 tu ya bajeti ya miradi ya maendeleo
  • Ni wizara iliyopata bajeti ndogo zaidi mwaka 2022/23
  • Bajeti ya mwaka 2023/24 yashuka zaidi, Kamati ya Bunge yasema haijaridhishwa

Dar es Salaam, Huenda azma ya Serikali ya kukuza, kuendeleza na kufanya mageuzi katika sekta ya sanaa na michezo nchini ikasalia kuwa ndoto mara baada ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo  kuidhinishiwa fedha kidogo kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zake.

Kati ya Sh35.4 bilioni zilizoombwa na wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2022/2023  ni  asilimia 45 tu ya fedha hizo zimetolewa na Serikali.

Naibu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo Husna Juma Sekiboko aliyekuwa akisoma uchambuzi wa bajeti uliofanywa na kamati hiyo leo Juni 6, 2023 amewaambia wabunge kuwa mpaka mwezi Februari 2023, Serikali imetoa jumla ya Sh19.3 bilioni pekee.

“Serikali imetoa  asilimia 33.6 ya fedha za mishahara zilizoombwa asilimia 35.1 ya fedha za matumizi mengineyo na asilimia 32 ya fedha za miradi na maendeleo zilizoidhinishwa,” amesema Sekiboko Bungeni jijini Dodoma.

Kwa mwaka 2022/23 bunge liliidhinisha Sh15.8 bilioni kwa ajili ya miradi ya maendeleo ambapo Serikali imetoa Sh5.2 bilioni pekee wakati zikiwa zimesalia siku chache tu kabla ya kuanza mwaka mpya wa fedha yaani Julai mosi.


Soma zaidi


Kwa mujibu wa kamati hiyo kiasi hicho ni kidogo ukilinganisha na majukumu ya Wizara hiyo ambayo ni kukuza, kulinda, na kuendeleza utambulisho wa mtanzania katika nyanja ya ubunifu, utamaduni, sanaa na michezo.

Ufinyu wa bajeti pamoja na kutotoa fedha kwa wakati ni miongoni mwa sababu zinazokwamisha utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika sekta hiyo.

Bajeti ya maendeleo 2023/24 yashuka

Pamoja na Wizara hiyo kupokea fedha chini ya asilimia 50 ya bajeti iliyoidhinishwa pamoja na asilimia 32 tu ya fedha za miradi ya maendeleo, fedha kwa ajili ya shughuli za maendeleo kwa mwaka 2023/24 imepungua kwa asilimia 25 kulinganisha na mwaka uliopita kutoka Sh15.8 bilioni hadi Sh11.8 bilioni.

“Kamati haijaridhishwa na hatua ya Serikali kupunguza bajeti ya miradi ya maendeleo, hatua hii haiendani kabisa na nia ya Serikali hususani maelekezo ya Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ya kukuza na kuimarisha sekta ya utamaduni na sanaa nchini  na haiakisi muamko wa Watanzania ya kupenda na kukumbatia sekta hii muhimu,” amesisitiza Sekiboko.

Ili kuiongezea nguvu wizara hiyo kufanya kazi ipasavyo, kamati imeishauri Serikali kuongeza fedha za miradi ya maendeleo angalau kuwa sawa na ya mwaka uliopita au zaidi.

Hivi karibuni sekta ya michezo na sanaa imekuwa na mwamko mkubwa kupitia ushiriki wa wanamichezo na wasanii katika mashindano na majukwaa mbalimbali na kuiwakilisha vyema nchi.

Mafanikio makubwa zaidi ya hivi karibuni ni pamoja na  Klabu ya michezo ya Yanga kushika nafasi ya pili katika Mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika, pamoja na Mtanzania Gabriel Geay kushinda nafasi ya pili katika mbio ndefu nchini Uingereza.

Kwa mwaka 2023/24 Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo imepanga kutumia Sh35.4 bilioni ambapo kati ya fedha hizo Sh23.4 bilioni ni kwa ajili ya mishahara na matumizi mengineyo na Sh11.8 ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Bajeti ya maendeleo ya wizara hiyo kwa mwaka ujao ni sawa na asilimia 0.04 ya bajeti ya Serikali katika shughuli za maendeleo ambayo ni zaidi ya Sh15 trilioni.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Nukta TV

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Nukta TV

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Nukta TV