WHO: Uviko-19 bado upo, unaendelea kuua watu

August 27, 2022 6:34 am · David
Share
Tweet
Copy Link
  • Yasema watu milioni 1 wamefariki kwa ugonjwa huo.
  • Yasisitiza kuongeza nguvu ya kutoa chanjo. 

Dar es salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dk. Tedros Ghebreyesus amesema watu hawapaswi kujisahau wala kuchukulia kama janga la Uviko-19 limeisha kwa sababu linaendelea kuua mamilioni ya watu duniani.

Dk Tedros aliyekuwa akizungumza na waandishi wa Habari jijini Geneva Uswisi, Agosti 25 mwaka huu amesema “hatuwezi kusema tunajifunza kuishi na Uviko-19 wakati watu milioni 1 wamekufa na Uviko-19 mwaka huu pekee.”

Amewaambia waandishi wa habari kuwa miaka miwili na nusu ya janga la Uviko-19 duniani “tuna nyenzo zote tunazohitaji za kuzuia vifo vitokanavyo na janga hili.”

Amezitaka serikali zote ulimwenguni kuimarisha juhudi zao za kutoa chanjo kwa wahudumu wote wa afya, wazee, na wengine walio katika hatari kubwa zaidi, mbinu hii ikiwa ni moja katika njia za kuweza kufikia utoaji wa chanjo ya Uviko-19 kwa asilimia 70 kwa watu wote ifikapo Desemba 2022.

“Inafurahisha kuona kwamba baadhi ya nchi zilizokuwa na viwango vya chini zaidi vya chanjo sasa zinainuka hususan barani Afrika,” amesema.

“Inafurahisha sana kuona kwamba utoaji chanjo unazingatia makundi yanayohitajika kupewa kipaumbele huku nchi nyingi zikipiga hatua ya kuvutia katika kutoa chanjo kwa asilimia 100 ya wafanyakazi wa afya na asilimia 100 ya wazee.”

Hata hivyo Dk Tedros amesema bado mengi zaidi yanahitajika kufanywa ili kutokomeza janga hilo la Afya ulimwenguni.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
7 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
7 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV