WHO: Mbu hawaenezi virusi vya Corona

June 8, 2020 8:55 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Shirika hilo limesema hakuna taarifa wala ushahidi kuthibitisha dhana hiyo. 
  • COVID-19 ni ugonjwa wa mfumo wa upumuaji unaotokana na maji maji wakati kupiga chafya au kukohoa. 
  • Kunawa mikono na kuvaa barakoa ndiyo kinga. 

Dar es Salaam. Kama wewe ni miongoni mwa watu ambao wanaamini ugonjwa wa virusi vya Corona unaenezwa na mbu, basi unajidanganya kwa sababu dhana hiyo haina ukweli wowote. 

Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema mpaka sasa hakuna taarifa wala uthibitisho unaoelezea kuwa virusi vya COVI-19 vinaweza kuenezwa kwa mbu.

Mbu ambao hung’ata wakati wa usiku hueneza ugonjwa wa malaria ambao kwa sasa ndiyo unaua watu wengi zaidi duniani. 

WHO imesema COVID-19 ni ugonjwa wa mfumo wa upumuaji ambapo maambukizi yake hutokea kwa maji maji yanayotoka mdomoni au puani kwa mtu mwenye ugonjwa huo.


Zinazohusiana.


Kwa kawaida maji maji hayo yanaweza kwenda kwa mtu mwingine kupitia kupiga chafya au kukohoa au kugusa mahali ambapo mtu mwenye ugonjwa huo alipigia chafya au kukoholea. 

“Epuka kukaa karibu na mtu yeyote anayekohoa na kupiga chafya,” imeeleza WHO kama njia ya kuepuka maambukizi ya COVID-19.

Njia nyingine ni kutumia vitakasa mikono (sanitizers) na kuosha mikono kwa sabuni na maji tiririka lakini kuvaa barakoa kila unapokwenda katika mikusanyiko ya watu. 

Kumbuka kuendelea kuchukua tahadhari na kufuata maelekezo ya wataalam wa afya kwa sababu Corona bado ipo.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.