Hapana: Wanaovaa miwani hawana uwezekano mdogo wa kupata Corona
- Hakuna tafiti rasmi iliyothibitisha madai hayo.
- Taarifa zinazosambaa juu ya madai hayo ya kuvaa miwani kujikinga na Corona siyo ya kweli.
- Watu washauriwa kupata sahihi za Corona kupitia WHO na Wizara ya Afya.
Dar es Salaam. Kama wewe ni mtumiaji wa miwani, huenda ulianza kujihisi mwenye bahati baada ya kukutana na taarifa zikidai kuwa watumiaji wa miwani wana uwezekano mdogo wa kuugua ugonjwa wa Corona.
Lakini huenda matarajio uliyonayo siyo sahihi kwa sababu taarifa hizo ambazo zinasambaa kwenye mitandao ya kijamii hazina ukweli wowote.
Habari hiyo inayosambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii ikiwemo Whatsapp na Twitter, kwa mfumo wa picha ya mtoto amevaa barakoa na miwani, imeambatanishwa na maandishi na kiunganishi kinachoelekeza kwenda kwenye taarifa husika.
Maandishi katika picha hiyo yanasema “Coronavirus: Glasses wearers less likely to get COVID.” yakimaanisha “Wavaaji wa miwani wana uwezekano mdogo wa kuugua Corona.”
Hata hivyo, habari hiyo haina ukweli wowote kwasababu hakuna tafiti yoyote rasmi iliyothibitisha madai hayo.
Pia tovuti inayochapisha machapisho ambayo hayajarasimishwa iitwayo Medrixiv imeeleza juu ya tafiti iliyofanyika India inayosema watumiaji wa miwani hawana asilimia kubwa ya kuugua Corona, lakini bado madai hayo yameonekana kuwa siyo ya kweli.
Madai kwenye tafiti hiyo yanaonekana kuwa sio kweli baada ya sehemu ya tafiti hiyo kusema “Preprints are preliminary reports of work that have not been certified by peer review. They should not be relied on to guide clinical practice or health-related behavior and should not be reported in news media as established information.”
Ujumbe huo unamaanisha “Machapisho yasiyo rasmi, yasitiliwe maanani na yasitumike na vyombo vya habari kama taarifa rasmi,”
Kwa mantiki hiyo, uvaaji wa miwani hakuweki salama dhidi ya Corona.
Zinazohusiana:
- Hapana: Kuosha pua kwa maji ya chumvi hakuzuii Corona
- Corona: Kitakasa mikono hiki hakina madhara ya kiafya
Watumiaji wa mitandao ya kijamii wanapaswa kutumia taarifa sahihi kutoka machapisho yaliyorasimishwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) ili kujikinga na COVID-19.
Baadhi ya tahadhari zinazopendekezwa za kujikinga ni kuvaa barakoa, kunawa mikono mara kwa mara, kutumia tishu wakati wa kukohoa au kupiga chafya na kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima.
Hata hivyo, WHO na jumuiya za kimataifa zimepiga hatua kudhibiti ugonjwa huo kwa kuanza kutoa chanjo mbalimbali chini ya programu maalum ya COVAX.
Latest
