Wanafunzi darasa la saba kuanza mtihani wa Taifa kesho

October 4, 2022 1:54 pm · Davis Matambo
Share
Tweet
Copy Link
  • Mitihani hiyo itafanyika kwa siku mbili Oktoba 5 hadi 6, 2022 nchi nzima.
  • Watahiniwa milioni 1.4 wa darasa la saba wanatarajia kuanza mitihani ya kumaliza elimu ya msingi kesho.

Dar es Salaam. Watahiniwa milioni 1.4 wa darasa la saba wanatarajia kuanza mitihani ya kumaliza elimu ya msingi kesho, ikiwa ni daraja muhimu kujiunga na sekondari. 

Kwa mujibu wa Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta) mitihani hiyo itafanyika kwa siku mbili Oktoba 5 hadi 6, 2022 nchi nzima.

Necta imesema kati ya watahiniwa hao, 723,064 ni wasichana sawa na asilimia 52 ya watahiniwa wote.

Idadi ya watahiniwa hao imeongezeka kwa asilimia 22 kutoka milioni 1.1 wa mwaka 2021.

“Aidha, jumla watahiniwa wenye mahitaji maalum ni 4,221, miongoni mwao 101 ni vipofu,  1,198 wasioona vizuri, viziwi 962, walemavu wa akili 487 na walemavu wa viungo 1,473,” amesema Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Athumani Amasi.

Mtihani huo utahusisha jumla ya masomo matano ambayo ni Hisabati, Sayansi na Teknolojia, Kiswahili, Lugha ya Kiingereza, na Maarifa ya Jamii.

Kwa mujibu wa Necta, ufaulu wa jumla wa wanafunzi katika matokeo ya darasa la saba mwaka jana ulikuwa 81.97 huku wanafunzi 393 walifutiwa matokeo.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.