Necta yatangaza matokeo ya darasa la saba 2022, ufaulu ukishuka kidogo

December 1, 2022 8:53 am · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ufaulu wa jumla umepungua kwa asilimia 2.3 ukilinganisha na mwaka jana.
  • Idadi ya watahiniwa waliofaulu imeongezeka kwa asilimia 18.24.

Dar es Salaam. Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya mtihani wa darasa la saba kwa mwaka 2022  huku ufaulu wa jumla ukipungua kwa asilimia 2.3 ikilinganishwa na mwaka jana.

Watahiniwa milioni 1.07  kati ya milioni 1.34 waliofanya mtihani huo wamefaulu sawa na asilimia 79.6.

Kaimu Katibu Mtendaji wa Necta, Athuman Amasi akitangaza matokeo hayo leo Desemba 1, 2022 Jijini Dar es Salaam amesema kati ya watahiniwa waliofaulu, wasichana ni 558,825 sawa na asilimia 79.9 ya wasichana waliofanya mtihani huo huku wavulana wakiwa ni 514,577.

“Kitakwimu kuna punguzo la ufaulu kwa asilimia 2.35 japokuwa kwa idadi ya watahiniwa waliofaulu imeongezeka kwa asilimia 18.24,” amesema Dk Amasi. 


Zinazohusiana


Watahiniwa milioni 1.38 wa shule za msingi walisajiliwa kufanya mtihani huo wakiwemo wasichana 723,027 sawa na asilimia 52.23 ya watahiniwa wote. 

Kati ya watahiniwa waliosajiliwa, watahiniwa wenye mahitaji maalum walikuwa 4,221.

“Watahiniwa milioni 1.35 sawa na asilimia 97.57 ya waliosajiliwa walifanya mtihani. Kati yao wasichana walikuwa 709,556 sawa na asilimia 98.14 na wavulana walikuwa 641,325 sawa na asilimia 97 ya waliosajiliwa” amesema Amasi wakati akitangaza matokeo hayo. 

Watahiniwa 33,305 sawa na asilimia 2.42  hawakufanya mtihani huo uliofanyika Oktoba 5 na 6 mwaka huu nchi nzima kutokana na sababu mbalimbal zikiwemo utoro na ugonjwa.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV