Utalii wa kimataifa kushuka kwa asilimia 30

March 27, 2020 3:39 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Shirika la Utalii Duniani (WTO) linasema idadi ya watalii wa kimataifa itashuka kwa kati ya asilimia 20 na 30 kutokana na kusambaa kwa ugonjwa wa virusi vya corona. 

Shirika hilo linasema mamilioni ya watu waliojariwa katika sekta ya utalii watakuwa katika hatari ya kupoteza kazi zao kutokana na mlipuko wa ugonjwa huo. 

Taarifa ya shirika hilo lenye makao yake mjini Madrid Uhispania iliyolewa jana (Machi 26, 2020) inaeleza kuwa kupungua kwa idadi ya watalii kutasababisha hasara zaidi ya dola za Marekani bilioni 300 (Sh693.7 trilioni) katika utalii wa kimataifa. 

Duru za kimataifa zinaeleza kuwa virusi hivyo vya corona vinaonekana kusababisha athari kubwa zaidi ikilinganishwa na majanga yaliyopita kwani mwaka 2009 dunia ilipokumbwa na mzozo wa kifedha utalii ulishuka kwa asilimia 4 na mwaka 2003 kulipokuwa na virusi vya SARS vilivyowauwa watu 774 kote duniani, utalii ulishuka kwa asilimia 0.4. 

Shirika hilo mwanzoni mwa mwaka lilikuwa limekadiria kukuwa kwa utalii duniani kwa kati ya asilimia tatu na nne ila lililazimika kufanya mahesabu yake upya mwezi huu wa Machi baada ya kushuhudia kusambaa kwa virusi vya corona.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Nukta TV

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Nukta TV

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV