Utafiti kutegua kitendawili cha wafanyabiashara kukwepa kodi Tanzania

March 12, 2021 9:22 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Serikali inakamilisha utafiti kuhusu visababishi vya kiwango cha chini cha uhiari wa walipakodi kusajili biashara zao, ulipaji wa kodi.
  • Mawakala kuanza kusimamia mashine za kukusanyia mapato (EFD)na siyo TRA. 

Dar es Salaam. Wakati Serikali ikitarajia kukusanya na  kutumia Sh36.3 trilioni katika bajeti ya mwaka wa fedha 2021/22, imesema inakamilisha utafiti wa kubaini visababishi vya kiwango cha chini cha ulipaji kodi kwa wakati na hiari hasa kwa wafanyabiashara wadogo Tanzania. 

Waziri wa Fedha na Mipango,  Dk Philip Mpango aliyekuwa  akisoma mpango na ukomo wa bajeti ya mwaka 2021/22 Machi 11 bungeni mjini Dodoma amesema katika fedha hizo, Sh23 trilioni zimetengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida  sawa na asilimia 63 ya bajeti yote.

Kati ya mapato yote yatakayokusanywa, ya ndani yanatarajiwa kuwa Sh26 trilioni sawa na asilimia 71.8 ya bajeti yote. 

Misaada na mikopo nafuu kutoka kwa washirika wa maendeleo (Sh2.9 trilioni), mikopo ya ndani (Sh5 trilioni) na mikopo ya nje yenye masharti ya kibiashara itakuwa Sh2.4 trilioni.


Zinazohusiana: 


Hata hivyo, katika kuhakikisha Serikali inakusanya kwa ukamilifu mapato ya ndani, imesema inakamilisha utafiti utakaosaidia kubaini sababu zinawafanya wafanyabiashara kutolipa kodi na kutoa taarifa sahihi kuhusu biashara zao.

“Serikali inakamilisha utafiti kuhusu visababishi muhimu vya kiwango cha chini cha uhiari wa walipakodi kusajili biashara zao, ulipaji wa kodi kwa wakati na uwazi katika utoaji wa taarifa sahihi kuhusu biashara wanazofanya, hususan kwa wafanyabiashara wadogo,” amesema Dk Mpango katika hotuba yake. 

Utafiti huo unahusisha kuchunguza changamoto za kitaasisi, tabia sababishi na hatua zinazopaswa kuchukuliwa ili kuongeza kasi ya ulipaji kodi nchini.

Aidha, Dk Mpango amesema Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inatekeleza mradi wa kurejesha jukumu kusimamia mashine za kukusanyia mapato (EFD) kwa mawakala  ili kuongeza ufanisi katika usambazaji wa mashine za EFD pamoja na utoaji wa huduma za kiufundi pindi mashine hizo zinapopata hitilafu. 

“Vile vile, Serikali inafanya mapitio ya mfumo wa mapato na matumizi kwa lengo la kuwezesha upatikanaji wa mapato yatakayokidhi ugharamiaji wa mahitaji ya Serikali na hivyo kuwa na bajeti endelevu,” amesema Dk Mpango. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV