Upungufu wa vyoo bado kitendawili Pangani
- Uwiano wa matundu ya vyoo kwa wanafunzi katika shule za msingi upo juu ya uwiano wa Kitaifa.
- Hali hiyo inawaweka wanafunzi hao hatarini kupata magonjwa ya mlipuko.
Dar es Salaam. Ripoti ya TakwImu Muhimu za Elimu 2020 (BEST 2020) zilizotolewa na Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) iinaonesha kuwa uwiano wa matundu ya vyoo kwa wanafunzi katika shule za msingi wilayani Pangani, mkoani Tanga upo juu zaidi ya uwiano wa Kitaifa, jambo linalowaweka hatarini wanafunzi hao.
Kwa mujibu wa takwimu hizo, tundu moja la choo linatumiwa na wanafunzi 38 kwa upande wa wavulana,ikiwa ni juu ya uwiano wa Kitaifa wa tundu moja kwa wavulana 25.
Kwa upande wa wasichana tundu moja la choo linatumiwa na wanafunzi 35, tofauti na uwiano wa Kitaifa wa tundu moja kwa wasichana 20.
Hali hiyo inawaweka hatarini wanafunzi kupata magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu na kuhara, ambayo yanaweza sababisha wanafunzi hao kutokuhudhuria darasani na kufanya vibaya kwenye masomo yao.
Latest
