Walimu bado changamoto shule za msingi Maswa
- Mwalimu mmoja anafundisha takriban wanafunzi 71 katika shule za msingi.
Dar es Salaam. Changamoto ya idadi ndogo ya walimu wa shule ya msingi, imeendelea kuitesa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa iliyopo Mkoani Simiyu.
Kwa mujibu wa Ripoti ya Takwimu Muhimu za Elimu (2021) zilizotolewa na Ofisi ya Rais Tamisemi, wilaya hiyo yenye wanafunzi wa shule za msingi 83,898, ina walimu 1,189 pekee, hali inayosababisha mwalimu mmoja kufundisha wanafunzi 71, kiwango ambacho ni juu ya uwiano wa Kitaifa wa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 45.
Changamoto inaongezeka zaidi kwa walimu wa kike ambao wapo 470 sawa na asilimia 39.5 ya walimu wote wa shule za msingi wilayani humo.
Hali hiyo inasababisha wanafunzi wa kike ambao wameanza kupata hedhi kushindwa kupata msaada wa karibu wawapo shuleni.

Latest