Hali halisi ya walimu shule za msingi Pangani

April 12, 2022 7:22 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Licha ya baadhi ya shule za msingi katika Wilaya ya Pangani mkoani Tanga kukabiliwa na uhaba wa walimu bado wilaya hiyo ina uwiano mzuri wa walimu kwa wanafunzi.

Kwa mujibu wa takwimu Muhimu za Elimu (BEST 2021) zilizotolewa na Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), mwalimu mmoja mwenye sifa wilayani humo anafundisha wanafunzi 51 kiwango ambacho ni juu ya uwiano wa kitaifa wa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 45.

Uwepo wa walimu wa kutosha shuleni unasaidia wanafunzi kupata maarifa na ujuzi kwa wakati.

 

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW