Upungufu wa vyoo bado kitendawili Pangani

February 15, 2022 8:19 am · Herimina
Share
Tweet
Copy Link
  • Uwiano wa matundu ya vyoo kwa wanafunzi katika shule za msingi upo juu ya uwiano wa Kitaifa.
  • Hali hiyo inawaweka wanafunzi hao hatarini kupata magonjwa ya mlipuko.

Dar es Salaam. Ripoti ya TakwImu Muhimu za Elimu 2020 (BEST 2020) zilizotolewa na Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais,  Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) iinaonesha kuwa uwiano wa matundu ya vyoo kwa wanafunzi katika shule za msingi wilayani Pangani, mkoani Tanga upo juu zaidi ya uwiano wa Kitaifa, jambo linalowaweka hatarini wanafunzi hao.

Kwa mujibu wa takwimu hizo, tundu moja la choo linatumiwa na wanafunzi 38 kwa upande wa wavulana,ikiwa ni juu ya uwiano wa Kitaifa wa tundu moja kwa wavulana 25.

Kwa upande wa wasichana tundu moja la choo linatumiwa na wanafunzi 35, tofauti na uwiano wa Kitaifa wa tundu moja kwa wasichana 20.

Hali hiyo inawaweka hatarini wanafunzi kupata magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu na kuhara, ambayo yanaweza sababisha wanafunzi hao kutokuhudhuria darasani na kufanya vibaya kwenye masomo yao.

 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA AKIHITIMISHA MAFUNZO YA UONGOZI NGAZI YA JUU, UONGOZI DARAJA LA PILI KOZI 2025/26

🔴LIVE: RAIS SAMIA AKIHITIMISHA MAFUNZO YA UONGOZI NGAZI YA JUU, UONGOZI DARAJA LA PILI KOZI 2025/26

Nukta TV

Rais Samia: Anzisheni mfuko  kuwasaidia wafungwa wenye ujuzi wanapotoka gerezani

Rais Samia: Anzisheni mfuko kuwasaidia wafungwa wenye ujuzi wanapotoka gerezani

Nukta TV

🔴LIVE: RAIS SAMIA AKIHITIMISHA MAFUNZO YA UONGOZI NGAZI YA JUU, UONGOZI DARAJA LA PILI KOZI 2025/26

🔴LIVE: RAIS SAMIA AKIHITIMISHA MAFUNZO YA UONGOZI NGAZI YA JUU, UONGOZI DARAJA LA PILI KOZI 2025/26

Nukta TV