Tahadhari: Mashine za kukaushia mikono haziui virusi vya Corona

July 13, 2020 6:09 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema mashine hizo siyo njia sahihi ya kuua virusi vya COVID-19.
  • Kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka mara kwa mara na kutumia vitakasa mikono inaweza kukusaidia kujikinga na ugonjwa huo. 

Dar es Salaam. Huenda wewe ni miongoni mwa watu ambao wanatumia mashine za kukaushia mikono hasa ukiwa katika vyoo au maeneo ya umma na umekuwa ukiamini kuwa mashine hizo zinaweza kuua virusi vya Corona. 

Fahamu wazi kuwa mashine hizo hazina uwezo wa kuua virusi hivyo aina ya COVID-19 na unachokiamini hakina ukweli wowote. 

Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema mashine hizo siyo njia sahihi ya kuua virusi vya COVID-19.

Limewataka watu kuendelea kuchukua tahadhari ya kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka mara kwa mara na kutumia vitakasa mikono (sanitizers). 

“Baada ya mikono yako kuwa safi, unaweza kuikausha kwa kutumia karasi laini au kukausha kwa mashine,” imeeleza WHO na kubainisha kuwa mashine za kukaushia mikono zitumie baada ya mtu kunawa mikono. 


Zinazohusiana


Kutokana na mashine kutumiwa na watu wengi kwenye maeneo ya umma zinaweza kuwa sehemu za kusambaza COVID-19 hasa kama zitaguswa.

Unakumbushwa usiguse mashine hiyo wakati wa kuitumia ili kujikinga na maradhi ya ugonjwa huo. 

Corona bado ipo, tuendelee kuchukua tahadhari.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.