Serikali yapendekeza kuondoa ada vyuo vya ufundi Tanzania

June 16, 2023 4:50 am · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni kwa ajili ya kuongeza wataalamu wenye ujuzi kuchochea mapinduzi ya viwanda.
  • Vyuo vinavyopendekezwa ni DIT, MUST, pamoja na ATC.

Dar es Salaam. Serikali inakusudia kuondoa ada katika ngazi ya elimu ya kati kwa baadhi ya vyuo vya umma nchini ili kuongeza idadi ya wataalamu wenye ujuzi unaohitajika katika mapinduzi ya viwanda yanayotarajiwa kuwa gurudumu la uchumi.

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba amewaambia wabunge jijini Dodoma kuwa katika jitihada za kuondoa ada kwa wanafunzi nchini anapendekeza sasa kuwaondolea karo wanafunzi watakaochaguliwa na Serikali kujiunga vyuo vya ufundi. 

Katika hotuba yake ya bajeti, Dk Nchemba vyuo vinavyopendekezwa kufutiwa ada ni  Dar es Salaam Institute of Technology (DIT), Mbeya University of Science and Technology (MUST) pamoja na Arusha Technical College (ATC).

“Napendekeza kuondoa ada kwa wanafunzi wanaomaliza kidato cha nne na kupangiwa na Serikali kujiunga na vyuo vya ufundi vya DIT, MUST  na ATC, hatua hii inalenga kuongeza idadi ya wataalamu wenye ujuzi na elimu inayohitajika katika azma hizi za mapinduzi ya nne ya viwanda,” amesema Dk Nchemba.


Soma zaidi


Kwa muda mrefu wadau wa mbalimbali wamekuwa wakiishauri Serikali kuondoa ada au kuweka utaratibu wa mikopo kwa wanafunzi wanaosoma vyuo vya kati jambo ambalo Mwigulu amesema Serikali inakusudia kutekeleza mwaka 2023/24.

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Nukta TV

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Nukta TV

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Nukta TV