Sababu Mbowe kugombea tena uenyekiti Chadema

December 21, 2024 4:34 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Asema hawezi kung’atuka wakati chama hicho kikiwa kwenye mivutano.

Arusha. Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe amesema atagombea tena uenyekiti wa chama hicho kwa kuwa bado kipo kwenye mivutano.

Mbowe ametoa uamuzi huo ikiwa ni saa 48 tangu aombe kupewa muda wa kutafakari kuhusu hatma ya nafasi hiyo ya unyekiti aliyohudumu katika miaka 20 iliyopita.

Kwa maamuzi hayo Mbowe anakuwa mtia wa tatu katika nafasi ya uenyekiti wa chama hicho akichuana vikali na Tundu Lissu pamoja na mgombea mwingine katika uchaguzi utakaofanyika Januari 2025.

Akizungumza na wanahabari pamoja na wanachama wa chama hicho leo Disemba 21, 2024 nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam Mbowe amesema kuwa alitamani sana kung’atuka katika nafasi hiyo lakini imeshindikana

“Nimetafakari kwa kina sana, nilitamani kuondoka lakini siwezi kuondoka katikati ya mivutano iliyopo, kwa hiyo Chadema nipo, nitakuwepo. Nitagombea,” amesema Mbowe. 

Kwa mujibu wa Mbowe miongoni mwa sababu zinazomfanya kugombea tena ni kuendelea kukipa nguvu chama hicho kuelekea kwenye uchaguzi mkuu huku kukiwa na changamoto za nyingi ikiwemo mifumo mibovu ya uchaguzi.

“Bado tuna matatizo mengi yanayohitaji ufumbuzi…tumeona uchaguzi wa juzi ulivyokuwa na mwaka ujao tuna uchaguzi, sisi Chadema tunasema ‘No reforms no elections’ tunaendelea kupambana na tutaendelea kudai katiba, mifumo huru ya uchaguzi na sheria za haki za uchaguzi,”amesema Mbowe.

Katika hatua nyingine Mbowe amewahakikishia wananchi kuwa chama hicho kitaendela kudumu hata akiondoka madarakani.

“Naona watu wengi wanapiga ramri Chadema inaenda kupasuka, inapasukia wapi? Huyu anayefikiria na kuiombea Chadema ife yeye siyo mwana Chadema…

…Hiki chama ni taasisi kamili hakitauwawa na Mbowe ama mtu mwingine yoyote kwa sababu hiki chama kimeenda zaidi ya kuwa chama cha Chadema na kuwa chama cha Watanzania.”amesema Mbowe.

Aidha, Mbowe amewataka wagombea wa uongozi wa ngazi ya Taifa ya chama hicho kufanya kampeni kwa haki na amani huku wakizingatia kukilinda kwani ni jukumu lao.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.