Lissu kugombea uenyekiti wa Chadema Taifa

December 12, 2024 12:38 pm · Esau Ng'umbi
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu amesema atawania uenyekiti wa chama hicho dhidi ya Mwenyekiti wake wa sasa Freeman Mbowe aliyekaa kwenye nafasi hiyo kwa miongo miwili.

Lissu ametangaza uamuzi huo leo Desemba 12, 2024 katika mkutano wake na wanahabari uliofanyika ukumbi wa Mlimani jijini Dar es Salaam ambapo amesema ameshawasilisha rasmi kusudio la kuwania nafasi hiyo kwa Katibu Mkuu wa Chadema.

“Napenda kuwajulisheni rasmi kwamba nimeshawasilisha taarifa rasmi kwa katibu mkuu wa chama chetu ya kuondoa kusudio langu la kugombea nafasi ya makamu mwenyekiti kwa upande wa Tanganyika nililowasilisha tarehe 6 Agosti 2024 na badala yake sasa nimewasilisha kwa katibu mkuu kusudio rasmi la kugombea nafasi ya mwenyekiti wa chama taifa katika uchaguzi ujao,” amesema Lissu.

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mikakati ya Serikali kuhakikisha walimu wa VETA wanapata ajira na mikopo

Mikakati ya Serikali kuhakikisha walimu wa VETA wanapata ajira na mikopo

Nukta TV

Mama Salama alivyombana Wanu kuhusu maslahi ya walimu wanaojitolea

Mama Salama alivyombana Wanu kuhusu maslahi ya walimu wanaojitolea

Nukta TV

Kwanini uchafuzi wa mazingira ni tishio kwa afya ya binadamu na uchumi

Kwanini uchafuzi wa mazingira ni tishio kwa afya ya binadamu na uchumi

Nukta TV